Zanzibar Insurance Corporation

Zanzibar Insurance Corporation ZIC provides quality insurance services to individuals, private and government institutions.

ZIC YASHIRIKI JUKWAA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) limeshiriki katika Jukwaa la Uwekezaji Zanz...
04/06/2026

ZIC YASHIRIKI JUKWAA LA UWEKEZAJI ZANZIBAR

Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) limeshiriki katika Jukwaa la Uwekezaji Zanzibar 2026 (Zanzibar Investment Summit 2026), lililofunguliwa rasmi leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika Hoteli ya Golden Tulip Airport, Zanzibar.

Jukwaa hilo la siku tatu limewakutanisha wawekezaji, taasisi za umma na binafsi pamoja na wafanyabiashara kutoka ndani na nje ya Tanzania kwa lengo la kupanua fursa za biashara na uwekezaji katika visiwa vya Zanzibar.

Ushiriki wa ZIC katika jukwaa hilo unaonesha dhamira ya dhati ya kuendelea kuwa mshirika muhimu katika kukuza mazingira salama ya uwekezaji kupitia huduma mbalimbali za bima zinazolinda mali, biashara na miradi ya uwekezaji dhidi ya majanga yasiyotarajiwa.

Katika miaka ya hivi karibuni, Zanzibar imeendelea kujijengea sifa k**a moja ya maeneo yenye mazingira rafiki ya uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki, hali iliyowezesha kuvutia zaidi ya miradi 800 ya uwekezaji yenye thamani ya zaidi ya dola za Marekani bilioni 9.

Mafanikio hayo yamechangiwa na sera na mageuzi mbalimbali ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji pamoja na kuimarika kwa huduma za bima zinazowapa wawekezaji uhakika na ulinzi wa shughuli zao za kiuchumi.

Kupitia maonesho ya huduma yanayokwenda sambamba na jukwaa hilo, ZIC imepata fursa ya kukutana na wadau wa uwekezaji na kuwapa elimu ya juu ya huduma zinazopatikana ZIC.

đź“… 04 Juni, 2026
📍 Golden Tulip Airport, Zanzibar

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ZIC, Bw. Ali Mzee Ali pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZIC, Bw. Jape Khamis wameshi...
23/05/2026

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ZIC, Bw. Ali Mzee Ali pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZIC, Bw. Jape Khamis wameshiriki katika hafla ya ufunguzi wa Jukwaa la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi iliyofanyika leo katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Zanzibar Airport.

Jukwaa hilo lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar limefunguliwa rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na linajumuisha shughuli mbali mbali ikiwemo kikao kazi cha siku 3 pamoja maonesho ya huduma kutoka taasisi za umma na binafsi za ndani na nje ya Zanzibar kwa lengo kuimarisha ushirikiano, uwajibikaji na kubadilishana uzoefu baina ya taasisi hizo.

Tukiwa miongoni mwa wadhamini wa jukwaa hilo muhimu, tunawakaribisha wananchi wote katika banda letu kwa ajili ya kupatiwa huduma za bima.

Wasiliana nasi kupitia:
Simu: 080 000 8005
WhatsApp: +255659072500
Baruapepe: [email protected] / [email protected]

Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) kupitia kampuni tanzu ya ZIC Takaful limeibuka mshindi wa tuzo ya Kampuni ya bima Inayoku...
23/05/2026

Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) kupitia kampuni tanzu ya ZIC Takaful limeibuka mshindi wa tuzo ya Kampuni ya bima Inayokua kwa Kasi Tanzania katika hafla ya utoaji wa tuzo za ATI Awards iliyofanyika jana katika ukumbi wa Superdome, Masaki jijini Dar es Salaam.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya bima nchini, wakiongozwa na Mgeni rasmi wa hafla hiyo ambae ni Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware pamoja na Naibu Kamishna wa Bima Tanzania Bi. Khadija Said, sambamba na viongozi na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali za bima.

Ushindi huu ni matokeo ya juhudi endelevu za kuboresha huduma za bima, kuongeza ubunifu katika bidhaa za bima pamoja na kujenga imani kwa wateja ndani na nje ya Zanzibar.

Tuzo hii ni heshima kubwa kwetu na inathibitisha ukuaji na mchango wetu katika maendeleo ya sekta ya bima nchini.

Wasiliana nasi kupitia:
Simu: 080 000 8005
WhatsApp: +255659072500
Baruapepe: [email protected] / [email protected]

Shirika la Bima la Zanzibar linatoa shukrani za dhati kwa Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar kwa kuandaa mkutano na waa...
21/05/2026

Shirika la Bima la Zanzibar linatoa shukrani za dhati kwa Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar kwa kuandaa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo katika Hoteli ya Golden Tulip Zanzibar Airport kuhusu maandalizi ya Jukwaa la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi.

Shirika la Bima la Zanzibar linajivunia kuwa miongoni mwa wadhamini wa jukwaa hilo muhimu linalolenga kuimarisha ushirikiano, uwajibikaji na kubadilishana uzoefu baina ya taasisi za umma na binafsi zitakazoshiriki.

Tunatoa pongezi kwa washiriki wote na vyombo vya habari kwa mchango wao katika kufanikisha maandalizi ya jukwaa hilo muhimu kwa maendeleo ya taasisi na taifa kwa ujumla.

Wasiliana nasi kupitia:
Simu: 080 000 8005
WhatsApp: +255659072500
Baruapepe: [email protected] / [email protected]

Tutashiriki katika Jukwaa la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma 2026 litakalofanyika kuanzia tarehe 23 hadi 2...
21/05/2026

Tutashiriki katika Jukwaa la Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma 2026 litakalofanyika kuanzia tarehe 23 hadi 25 Mei, 2026 katika Hoteli ya Golden Tulip Airport.

Wasiliana nasi kupitia:
Simu: 080 000 8005
WhatsApp: +255659072500
Baruapepe: [email protected] / [email protected]

ZIC tutashiriki katika “KLINIKI YA HUDUMA YA PAMOJA KWA DIASPORA WA TANZANIA NCHINI NETHERLAND”📍The Hague, Netherlands.📆...
06/05/2026

ZIC tutashiriki katika “KLINIKI YA HUDUMA YA PAMOJA KWA DIASPORA WA TANZANIA NCHINI NETHERLAND”

📍The Hague, Netherlands.
📆 08 May hadi 10 May 2026.

Tunawatakia mitihani mema ya kidato cha sita 2026.Wasiliana nasi kupitia:Simu: 080 000 8005WhatsApp: +255659072500Baruap...
04/05/2026

Tunawatakia mitihani mema ya kidato cha sita 2026.

Wasiliana nasi kupitia:
Simu: 080 000 8005
WhatsApp: +255659072500
Baruapepe: [email protected] / [email protected]

Timiza ndoto yako na ZIC Wakala. Kuwa sehemu ya kufikisha huduma bora za bima kwa wateja wetu. Wasiliana nasi leo uweze ...
04/05/2026

Timiza ndoto yako na ZIC Wakala. Kuwa sehemu ya kufikisha huduma bora za bima kwa wateja wetu.

Wasiliana nasi leo uweze kujiunga na ZIC wakala:-
Simu: 080 000 8005
WhatsApp: +255659072500
Baruapepe: [email protected] / [email protected]

Address

Maisara/Mpirani
Zanzibar
255

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00
Saturday 08:00 - 12:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibar Insurance Corporation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share