Viungo Project

Viungo Project VIUNGO PROJECT is a project aimed to unlock the potential of the horticulture value chain, increas

Katibu mkuu wizara ya kilimo Zanzibar,  Seif Shaban (kulia) na Anna Constantini, afisa kutoka  wakikagua shamba la Vanil...
10/06/2023

Katibu mkuu wizara ya kilimo Zanzibar, Seif Shaban (kulia) na Anna Constantini, afisa kutoka wakikagua shamba la Vanilla la kikundi cha Vanilla Growing Cooperative katika Shehia ya Donge Mbiji, wilaya ya Kaskazini B ambao ni wanufaika wa unaotekelezwa kupitia program ya ๐Ÿ‡ช๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ wakati wa ziara ya maafisa wa Wizara hiyo, maafisa wa Umoja wa Ulaya pamoja na timu ya wataalam washauri kutembelea na kutathimini maendeleo ya program hiyo kwa wanufaika katika sekta ya kilimo.

"Tushirikiane na wakulima katika masuala ya masoko ili kuhakikisha wanapata masoko bora kwaajili ya kuuza bidhaa zao kwa bei ya faida hasa kwa mazao ya viungo," ameeleza Katibu Mkuu huyo.

European Union in Tanzania
https://www.instagram.com/p/CtTyZ6ktghq/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==

ZIARA ya maafisa wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar na wataalam kutoka kwenye miradi inayote...
28/02/2023

ZIARA ya maafisa wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar na wataalam kutoka kwenye miradi inayotekelezwa chini ya mpango wa ๐Ÿ‡ช๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ kwa ufadhili wa European Union in Tanzania inaendelea kisiwani Pemba kwa siku ya pili.

Katika ziara hiyo inayoongozwa na Afisa mkuu wa Utafiti kutoka Wizara hiyo, Dkt. Suleiman Shehe, leo Februari 28, wametembelea wanufaika mbalimbali wa mradi wa unaotekelezwa na , , ambao ni wakulima na wasindikaji wa mazao ya kilimo na kupata picha halisi ya mwenendo wa utekelezaji wa shughuli za mradi huo katika kufikia lengo la kukuza mnyororo wa thamani kwa mazao ya Viungo, mboga na matunda.

Wakiwa katika ziara hiyo, wanufaika wa miradi iliyo chini ya programu ya ๐Ÿ‡ช๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ wamehimizwa kuzingatia suala la uwekaji kumbukumbu ya shughuli zao ili kujua gharama za uendeshaji na faida zake kwenye shughuli hizo.




https://www.instagram.com/p/CpM2HBKtHuu/?igshid=MWMzM2Q4ZmE=

Leo November 5/ 2022 K**ati ya ushauri utekelezaji Mradi wa Viungo Zanzibar  (ZMAG) wanakutana katika ofisi za utekeleza...
05/11/2022

Leo November 5/ 2022 K**ati ya ushauri utekelezaji Mradi wa Viungo Zanzibar (ZMAG) wanakutana katika ofisi za utekelezaji mradi huo Mwanakwerekwe mjini Unguja kwa lengo la kujadili kwa pamoja namna ya utekelezwaji mradi huu kwa miaka miwili iliopita nyuma, kutazama mafanikio na changamoto katika kipindi chote kisha kwa pamoja watashauri namna bora zaidi kuongeza kasi ya mafanikio katika utekelezaji mradi huo ili wananchi walio wengi waweze kunufaika.Mkutano huu unaongozwa na Mwenyekiti wake Mohamed K.Rashid.

Mradi wa Viungo unajihusisha na kilimo cha mboga mboga, matunda, na viungo (Spice) unatekelezwa kwa pamoja na taasisi ya People Development Forume (PDF) Tanzania Media Women Association (TAMWA-ZNZ) pamoja na Community Forest in Pemba (CFP) kwa mashirikiano na Umoja wa Ulaya (EU)

Makamo wa pili wa Rais Zanzibar, Mhe.  Hemed Suleiman tayari amezindua wiki ya maonesho Siku ya Chakula Duniani kisiwani...
10/10/2022

Makamo wa pili wa Rais Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman tayari amezindua wiki ya maonesho Siku ya Chakula Duniani kisiwani Pemba.

Tayari watu mbalimbali wakiwemo wanafunzi wamechangamkia fursa ya kujifunza Mbinu bora za kilimo cha Bustani za nyumbani kupotia lililopo ndani ya maomesho haya.

Karibu sana kwenye banda letu la ujifunze mbinu za KILIMO HAI uweze kunufaika na Jasho lako Shambani.

European Union in Tanzania


https://www.instagram.com/p/Cjh5JIPNl-8/?igshid=MDJmNzVkMjY=

MATUKIO KATIKA PICHA- SIKU YA 01: Maafisa wa Mradi wa VIUNGO wakitoa maelezo kwa wananchi waliofika kwenye banda letu la...
10/10/2022

MATUKIO KATIKA PICHA- SIKU YA 01:

Maafisa wa Mradi wa VIUNGO wakitoa maelezo kwa wananchi waliofika kwenye banda letu la maonesho ya Siku ya Chakula Duniani yaliyozinduliwa leo kisiwani Pemba na Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman.

Ewe mkulima njoo tupo hapa tunakusubiri wewe tu. Ukifika hakikisha unafika kwenye eneo letu la ujifunze kulima Viungo, mboga na matunda Kisasa ili kuondokana na umasikini katika familia yako.

European Union in Tanzania


https://www.instagram.com/p/CjiH765t2zC/?igshid=MDJmNzVkMjY=

Waziri wa Nchi ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Mhe. Harusi Said Suleiman (kushoto) akipokea maelezo ya kitaa...
10/10/2022

Waziri wa Nchi ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Mhe. Harusi Said Suleiman (kushoto) akipokea maelezo ya kitaalam kutoka kwa maafisa Mradi wa VIUNGO alipotembelea banda letu la kwenye maonesho Siku ya Chakula Duniani kisiwani Pemba mapema leo.

Bado unasuniri nini?... Ni zamu yako sasa NJOO tukifundishe mbinu mpya kabisa za kilimo cha Matunda, Mboga na Viungo.

by European Union in Tanzania

BADO SIKU 05  SIku zimebaki chache, na kila kitu kipo tayari kwaajili yako Mkulima wa Viungo, Mboga na Matunda  .   chin...
05/10/2022

BADO SIKU 05

SIku zimebaki chache, na kila kitu kipo tayari kwaajili yako Mkulima wa Viungo, Mboga na Matunda . chini ya imejiandaa vyema kutupatia mbinu mpya na bora za kilimo.

Yote haya utajifunza utakapofika kwenye Banda letu la ndani ya viwanja vya Maonesho Chamanangwe kisiwani Pemba kuanzia Octoba 10 -16, 2022.

European Union in Tanzania

MAONESHO SIKU YA CHAKULA DUNIANI YANAKUSUBIRI WEWE MKULIMA.BADO SIKU 07 TU.   Wataalam wetu wa Kilimo wapo tayari kuzung...
03/10/2022

MAONESHO SIKU YA CHAKULA DUNIANI YANAKUSUBIRI WEWE MKULIMA.

BADO SIKU 07 TU.

Wataalam wetu wa Kilimo wapo tayari kuzungumza na kila mkulima atakayefika kwenye Banda letu la Maonesho ya Kilimo Chamanangwe Pemba.

K**a una tatizo au swali lolote linalohusu Masuala ya kilimo iwe unasumbuliwa na Wadudu Shambani, Uzalishaji wako haukuletei Faida na Hujui namna Bora ya Kulima Kilimo HAI chenye kuzingatia mabadiliko ya , hakikisha kuanzia 10 Octoba-16 unafika katika Banda letu la kwenye maonesho Pemba ili kupata suluhisho lako.

unapewa nguvu na European Union in Tanzania


https://www.instagram.com/p/CjPu28WAfi9/?igshid=MDJmNzVkMjY=

WAKULIMA WAPATIWA MBINU ZA KUSARIFU MBOGA, MATUNDA.Wakulima wa bustani za nyumbani kutoka Shehia ya Maziwang'ombe, Wilay...
07/09/2022

WAKULIMA WAPATIWA MBINU ZA KUSARIFU MBOGA, MATUNDA.

Wakulima wa bustani za nyumbani kutoka Shehia ya Maziwang'ombe, Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wamepatiwa mafunzo ya kusarifu Nyanya na Mchicha kwa njia ya vitendo ikiwa ni utekelezaji mradi wa Viungo unaotekelezwa kupitia mpango wa kwa ufadhili wa European Union in Tanzania

Mafunzo hayo kwa wakulima yaliyoongozwa na Afisa Lishe na Uhakika wa Chakula wa mradi huu, Mkombozi Christopher Nzoya, yamelenga kupunguza upotevu wa mbogamboga msimu wa mavuno kwa jamii, kuhamasisha jamii kuacha kulima bustani za nyumbani kwa mazoea na badala yake kuwajengea uwezo wa kuzalisha bustani za nyumbani kwa dhamira ya kuboresha lishe ya familia na biashara.

Aidha mafunzo hayo pia yamelenga kuongeza matumizi sahihi ya lishe za mboga na matunda kwenye kaya katika msimu usio wa kilimo cha mazao hayo, ikiwa ni sambamba na kupunguza na kuzuia changamoto za utapiamlo zinazotokana na ukosefu wa Mboga za majani na matunda kwa watoto, wajawazito, wasichana wanaopevuka pamoja na akinamama wanaonyonyesha.


https://www.instagram.com/p/CiM3kn6NgrJ/?igshid=MDJmNzVkMjY=

Wakulima wanufaika wa   katika Shehia ya Vitongoji, Wilaya ya Chake chake mkoa wa kusini Pemba wanaendelea kutabasamu na...
31/08/2022

Wakulima wanufaika wa katika Shehia ya Vitongoji, Wilaya ya Chake chake mkoa wa kusini Pemba wanaendelea kutabasamu na kaulimbiu ya hii ikiwa ni kutokana na manufaa wanayopata kwasasa kupitia kilimo cha Nyanya ambapo wanaendelea kuvuna huku wakiwa na uwezo wa kuvuna na kuuza Ndoo 60-70 kwa siku kwasasa.

Mradi wa Viungo unatekelezwa kwa mashirikiano ya , na kupitia mpango wa kwa ufadhili wa European Union in Tanzania
https://www.instagram.com/p/Ch64TxGN2LV/?igshid=MDJmNzVkMjY=

Address

Zanzibar City

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Viungo Project posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Viungo Project:

Share