16/07/2023
HISTORIA YA BITCOIN TOKA MWAKA 2008 MPAKA SASA
INAENDELEA..
kwa bitcoin alizokuwa
nazo elfu kumi ni sawa na kwamba pizza hiyo ilifikia thamani ya
dola za Marekani milioni mia moja tisini na saba na nukta nane
tatu ($ 197.83 milioni). Malipo hayo yamebaki historia mpaka
sasa. Anajutiaje? Wengi wanasema aliidharau, je angetunza hizo
bitcoin basi angekuwa sehemu ya matajiri wakubwa duniani.
Tangia wakati huo bitcoin bado haikupata umaarufu wala
kujulikana sana. Mpaka kuanzia miaka ya 2010 hadi 2015 bitcoin
ikawa inatumika katika biashara haramu k**a za madawa ya
kulevya. Mtandao huo wa biashara haramu ulijulikana k**a Silk
Road, ulishamiri sana huko Marekani na ukawa muhimu kwa
sababu malipano yalifanyika kwa siri sana kati ya mtu na mtu na walilipana bila kujuana na ilikuwa sio rahisi kwa serikali kuingilia
na kuwajua wahusika. Bitcoin ilikuwa na uwezo wa kununua kila
kitu na bidhaa yoyote kupitia mtandao huo. Mpaka serikali ya
Marekani ilipokuja kugundua na mtandao huo kuvunjwa rasmi.
Hata hivyo biashara hiyo ilikuwa na matokeo rasmi mawili.
Moja, kwa mtandao huo wa bitcoin kutumika katika biashara
haramu basi ikavuma kwamba bitcoin imezaliwa kuwa pesa ya
kihuni, ya majambazi, ya wahalifu na magaidi. Hasa kwa sababu
mtandao huo wa Silk Road uliweza pia kutumia bitcoin kulipia
magaidi wa kujitoa mhanga na kununua silaha kwa shughuli za
mashambulizi ya kigaidi. Tukio hilo lilisababisha kuyumba sana
kwa bitcoin, na kujengewa picha hasi katika jamii.
Mbili, ikawa faida kwa bitcoin. Kwa sababu ya kuhusianishwa na
matukio ya kihalifu na biashara halamu, basi ikapelekea bitcoin
kutangazwa sana katika vyombo vya habari duniani kote.
Itaendelea follow ukurasa Kwa muendelezo zaidi