01/02/2025
🖱It's Finally Neymar amerejea Brazil👑
Baada ya kuvuna mabilioni ya fedha kwenye soka la Ulaya, Neymar Jr ameamua kurejea kwenye klabu iliyomlea—Santos FC.
Kabla ya utambulisho wake, alipiga goti k**a ishara ya heshima na kumuomba Mungu.
Thread: ⤵️
Kisha, huku machozi yakimtoka, akaibusu nembo ya Santos na kurudia ushangiliaji wake wa enzi zile.
Hii ni hadithi ya kilele na mwisho wa safari ya nyota mmoja wa zama hizi.
Wapenda soka wengi hawajafurahia uamuzi wa Neymar. Lakini at the end of the day we care about his happiness.
Madhabiki walitamani bado awe Ulaya, akipigania nafasi yake ya kuwa miongoni mwa wanasoka wakubwa.
Tangu akiwa kinda, watu waliamini angeweza kushinda Ballon d'Or angalau mara moja. 🔥
Je, nini kilikwamisha ndoto hiyo?
✅ Barcelona 2013-2017
Alipotua Camp Nou, alikuwa kipaji safi. Lakini kivuli cha Lionel Messi kilimfanya asitawale kikamilifu.
✅ PSG 2017-2023
Alipoenda PSG, alitaka kuwa mfalme wa timu. Lakini baada ya miaka miwili, ujio wa Kylian Mbappé ulibadili mpango mzima.
Baada ya hapo, alihisi kutengwa na klabu ikaanza kujengwa kumzunguka Mbappé.
Tatizo kubwa likawa majeraha.
Kati ya misimu 6 aliyocheza PSG, alikosa 53% ya mechi kwa sababu ya majeraha!
⚠️ 2018: Majeraha yakamfanya akose mechi muhimu vs Man United (UCL)
⚠️ 2019: Alikosa Copa América, Brazil wakashinda bila yeye
⚠️ 2021-2023: Mechi nyingi alizocheza zilikuwa chache sana kumlinganisha na nyota wa kiwango chake
Hatimaye, PSG walichoka, naye akaamua kuondoka.
Akachagua Saudi Pro League, akijiunga na Al-Hilal kwa mkataba wa €300M kwa miaka miwili. 💰
Lakini majeraha bado yakamuandama. Katika mechi 9 pekee, alifunga bao 1 na kutoa assist 3.
Baada ya jeraha lingine kubwa, Al-Hilal wakaamua kuvunja mkataba wake.
Ndoto ya kuendelea kutamba duniani ilizimika kabisa.
Wanadamu hawana huruma.
Watu wakaanza kusema: "Wabrazil ndivyo walivyo—wanapenda sana starehe!" 😏
Lakini Neymar si wa kwanza:
🇧🇷 Ronaldinho: Alipoanza kupungua makali, Barcelona walimtema haraka.
🇧🇷 Kaká: Alishinda Ballon d'Or 2007, lakini majeraha yalimmaliza.
🇧🇷 Ronaldo Nazário: Aliumia vibaya, lakini bado akarudi kushinda Kombe la Dunia 2002.
Kwa Neymar, hakukuwa na kurudi tena.
Wanasema ukikosa kila sehemu, rudi nyumbani.
Neymar amerudi Santos FC akiwa shujaa. Hapa hatakuwa na presha ya kushindana na Mbappé, Haaland, au Vinícius Jr.
Ni k**a kustaafu kwa heshima.
⚽️ Anaondoka bila Ballon d’Or
⚽️ Anaondoka bila Kombe la Dunia
Lakini anaondoka akiwa na historia ya mmoja wa wanasoka wenye kipaji cha kipekee kuwahi kutokea!
Katika historia ya soka, kuna wachezaji wachache waliofanikiwa k**a Neymar:
🏆 29 trophies
⚽️ 436 club goals
🎯 270+ assists
💰 Mchezaji ghali zaidi duniani (€222M 2017, PSG)
🌎 Mchezaji wa pili mwenye magoli mengi kwa Brazil (79), nyuma ya Pele (77)
Kwa wengi, Neymar hatakuwa katika hadhi ya Messi au CR7, lakini ubunifu wake ulibadilisha mchezo wa soka.⤵️
Neymar aliwapa mashabiki wa soka:
✅ Mbinu kali za dribbling 🎭
✅ Ubunifu wa hali ya juu 🧠
✅ Magoli ya kiufundi 🎯
✅ Sense of humor uwanjani 😂
Huwezi kumzungumzia soka la karne ya 21 bila Neymar.
Ni msanii aliyepaka rangi mchezo wa mpira wa miguu! 🎨
Asante kwa burudani, Neymar da Silva Santos Júnior. 🏆🔝
Hatujakusahau, na hatutakusahau. 🙌