30/05/2024
Habari yako Mtu wa Mungu!
Natumaini U Mzima?😊
Naitwa Henry, ni Mtumishi wa Mungu kutokea chuo cha umisheni cha Sayuni, Kilichopo Dar es Salaam.
Katika fumbo hili tunaona kuna mvuvi, bahari, nyavu / juya, samaki na chombo cha kubebea samaki wazuri.
Je fumbo hili linawahusu samaki au fumbo hili lawahusu watu waishio duniani?
HABAKUKI 1:14
"na kufanya wanadamu kuwa k**a samaki wa baharini, k**a vitu vitambaavyo, ambavyo havina mtawala”.
Kumbe Watu wamefananishwa na samaki katika Biblia, kwa maana hiyo fumbo hili linazungumzia watu na si samaki, watu hawa wako baharini.
Je bahari ni nini?
Ikiwa Samaki = watu, basi pia bahari imetumika k**a fumbo.
AMOSI 8:12
“12Nao watatangatanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huku na huko, kulitafuta neno la BWANA, wasilione.”
Je watu hutafuta neno baharini?? hapana
Je kwahiyo bahari ni nini??
Ni matumaini kuwa unatamani kujua zaidi..
Maana ya mvuvi,
Maana ya nyavu,
Maana ya juya,
Maana ya bahari, na
Maana ya chombo pia.
Napenda kukualika katika mafunzo haya ya Biblia ambayo utapata kufahamu mengi kuhusu Mafumbo, Unabii na Utimilifu na Kitabu Cha Ufunuo.
Mafunzo haya huwa ni siku 4 Tu Kwa wiki (J3, J4, Alh & Ijum)
Muda:
Saa 3 hadi 5 Asubuhi au
Saa 1 hadi 3 Usiku
Unaweza kufika Katika vituo vyetu vilivyopo
Mwananyamala, Kimara, Kigamboni, Mbagara au Tabata
Yohana 17:3. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
👉FURSA YA KUJIUNGA NA CHUO CHA BIBLIA NI KWAAJILI YA WOTE (WACHUNGAJI WA MADHEHEBU MBALIMBALI, MASHEMASI, WAINJILISTI, NA WASHIRIKA AU WAUMINI WOTE) NJOO UKUTANE NA NENO LILILOFUNULIWA KTK HUU UJIO WA PILI WA YESU KRISTO.
NB:
HAKUNA ADA WALA MALIPO YOYOTE
0620150540