Car and General Trading Ltd

Car and General Trading Ltd This is the official page for TVS Motorcycles in πŸ‡ΉπŸ‡Ώ. Sole Distributor: Car & General Tanzania Ltd

Tarehe 22 Agosti 2026, Car & General Tanzania iliunga mkono Tamasha la Madereva wa Pikipiki na Tuk Tuk lililoandaliwa na...
26/08/2026

Tarehe 22 Agosti 2026, Car & General Tanzania iliunga mkono Tamasha la Madereva wa Pikipiki na Tuk Tuk lililoandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Madereva wa Pikipiki na Tuk Tuk Msasani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, lenye kauli mbiu: β€œKwa Pamoja Tunafurahi, Karibu AFCON Msasani.”

Tamasha hilo lililenga kuikaribisha AFCON Msasani huku likikuza umoja, mshikamano na ushirikiano kati ya madereva na Jeshi la Polisi, pamoja na kuchangia katika kuimarisha sekta ya usafirishaji na usalama katika jamii.

Washiriki walifurahia michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mbio za magunia, kukimbiza kuku na michezo mingine ya burudani.

Akizungumza wakati wa tamasha hilo, Mgeni Rasmi, Diwani wa Kata ya Msasani, Mh. Yusuph Hamisi Yusuph, aliwahamasisha viongozi wa Shirikisho kuendelea kuandaa matukio ya aina hii, akisisitiza kuwa michezo ni chachu ya kujenga jamii yenye umoja, mshikamano na usalama.

Car & General Tanzania-Tunaamini katika maendeleo ya jamii.

Una swali kuhusu TVS?Tuko tayari kukusaidia.Chati nasi WhatsApp kwa huduma, maswali ya bidhaa, vipuri na maelezo zaidi.W...
26/08/2026

Una swali kuhusu TVS?

Tuko tayari kukusaidia.Chati nasi WhatsApp kwa huduma, maswali ya bidhaa, vipuri na maelezo zaidi.

WhatsApp: 0777 716 615
Piga simu: 0750 011 700

Tupo kila kona ya Tanzania kukupatia huduma bora zaidi.Piga simu: 0750 011 700 au 0674 711 111.
22/08/2026

Tupo kila kona ya Tanzania kukupatia huduma bora zaidi.

Piga simu: 0750 011 700 au 0674 711 111.

21/08/2026

Tamasha la Kihistoria kwa Madereva wa Pikipiki na TukTuk linakuja! πŸοΈπŸ›Ίβš½

Car & General Tanzania pamoja na TVS Tanzania, kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Madereva wa Pikipiki na TukTuk pamoja na Jeshi la Polisi, wamefanya mkutano na waandishi wa habari kuelekea tamasha kubwa litakalowakutanisha maafisa usafirishaji, Jeshi la Polisi na wadau mbalimbali wa michezo.

πŸ“ Uwanja wa Magunia, Msasani
πŸ—“οΈ 22 Agosti 2026
⏰ Kuanzia saa 04:00 asubuhi

Ni siku ya kujenga mshikamano, kuimarisha ushirikiano na kuleta jamii pamoja kupitia michezo. 🀝⚽

Car & General Tanzania na TVS Tanzania tunawaalika wote kushiriki na kuifanya siku hii kuwa ya kipekee!

21/08/2026

Village Califonia palikuwa moto! πŸ”₯🏍️

Tulijumuika pamoja na wateja wetu na familia zao katika HLX Day, siku maalum ya kusherehekea, kuungana na muhimu zaidi, kuonesha jinsi tunavyothamini na kutambua sapoti kubwa wanayotupatia kila siku.

Ilikuwa siku ya furaha, michezo, burudani na kumbukumbu nzuri pamoja.

Asanteni kwa kuwa sehemu ya safari yetu. Pamoja tunasonga mbele!

Car & General Tanzania na TVS Motor, ilishiriki katika Zoezi la Uchangiaji Damu la Viongozi (Executive Blood Drive) lili...
21/08/2026

Car & General Tanzania na TVS Motor, ilishiriki katika Zoezi la Uchangiaji Damu la Viongozi (Executive Blood Drive) lililoandaliwa na Africa Initiative Development Foundation (AIDF Tanzania), lenye lengo la kuchangia juhudi za kuimarisha upatikanaji wa damu na kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Zoezi hilo lilizinduliwa rasmi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chemba ya Taifa ya Biashara (TNCC), Bw. Oscar Kissanga, ambaye alihimiza viongozi na taasisi mbalimbali za serikali na zisizo za serikali kushiriki kikamilifu katika kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuchangia damu.

Katika uzinduzi huo, Bw. Kissanga alieleza kuwa wastani wa mahitaji ya damu nchini ni takribani unit 648,000 kwa mwaka, zinazohitajika kusaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto, waathirika wa ajali na wagonjwa wengine wanaohitaji damu kwa dharura.

Tushirikiane kuchangia damu. Kila tone linaweza kuokoa maisha.

Nyumbani, sokoni, kazini au shuleni, TVS King ipo tayari kukusogeza mbali zaidi kwa matumizi mazuri ya mafuta.Mafuta kid...
20/08/2026

Nyumbani, sokoni, kazini au shuleni, TVS King ipo tayari kukusogeza mbali zaidi kwa matumizi mazuri ya mafuta.
Mafuta kidunchu, umbali mrefu zaidi.

Piga simu: 0750 011 700 au 0674 711 111.

19/08/2026

Huduma Bure, Tabasamu Zaidi! 🏍

Car & General Tanzania kwa kushirikiana na TVS Motor imefanikiwa kutoa huduma za matengenezo bure kwa madereva wa bodaboda wa TVS katika Wilaya ya Temeke.

Tunaendelea kuwa karibu na madereva wetu kwa kuhakikisha wanapata huduma bora na pikipiki zao zinaendelea kufanya kazi kwa ufanisi.

Karibu Car & General, karibu uwe sehemu ya tabasamu la familia ya TVS!

TabasamuLaTVS

Tarehe 15 Agosti 2026, Car & General iliungana na maafisa usafirishaji pamoja na familia zao katika maadhimisho ya HLX D...
19/08/2026

Tarehe 15 Agosti 2026, Car & General iliungana na maafisa usafirishaji pamoja na familia zao katika maadhimisho ya HLX Day yaliyofanyika Village Califonia, Wazo, Tegeta.

Siku hii maalum ilikuwa ni fursa ya kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa maafisa usafirishaji katika kujenga taifa letu kupitia kazi zao za kila siku.

Mbali na kutambua juhudi zao, HLX Day 2026 iliambatana na michezo mbalimbali, burudani na shughuli za kijamii zilizolenga kuimarisha umoja, mahusiano na furaha miongoni mwa washiriki.

Car & General inaendelea kuwa bega kwa bega na maafisa usafirishaji, kuwapatia bidhaa bora, huduma zenye kuaminika na kuunga mkono shughuli zao za kila siku.

Changia damu okoa maisha ya mama na mtoto.Car & General Trading Limited na TVS Motor kwa kushirikiana na Africa Initiati...
17/08/2026

Changia damu okoa maisha ya mama na mtoto.

Car & General Trading Limited na TVS Motor kwa kushirikiana na Africa Initiative Development Foundation (AIDF), waliandaa kambi ya siku mbili ya uchangiaji damu katika Viwanja vya Buliaga, Temeke, yenye lengo la kusaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Kambi hiyo iliambatana na huduma bure za pikipiki za TVS, pamoja na huduma nyingine za afya, ikiwemo uchunguzi wa macho, afya ya kichwa na huduma nyingine muhimu kwa jamii.

Kupitia juhudi hizi, tunaendelea kutekeleza dhamira yetu ya kuleta tabasamu kwa kuwajibikwa kwa jamii inayotuzunguka.

ChangiaDamuOkoaMaisha

Address

Azikiwe Maktaba Street
Dar Es Salaam
1552

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 15:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Car and General Trading Ltd posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Car and General Trading Ltd:

Shortcuts

Share