PASS Trust ni Asasi ya kusaidia sekta binafsi ya kilimo iliyoanzishwa mwaka 2000 ili kuchochea uwekezaji na kukuza kilimo cha biashara na sekta zinazohusika. Ilisajiliwa mwaka 2007 k**a asasi isiyokuwa ya serikali kwa mujibu wa sheria ya ushirikishaji wadhamini ya mwaka 2002. DIRA
Kuwa asasi inayoongoza katika utoaji wa huduma za fedha na maendeleo ya biashara katika sekta ya kilimo. DHAMIRA
PASS
TRUST/Asasi ya PASS inawajibika katika utoaji wa huduma za maendeleo ya kilimo cha biashara na fedha kwa wafanyabiashara wajasiriamali wadogo na wa kati kwa kuwaunganisha katika tasisi za fedha. MALENGO
Malengo ya PASS ni kuchochea uwekezaji na kuhimiza ukuaji wa kilimo nchini Tanzania. Huduma zinatotolewa na PASS ni:
1. Huduma za maendeleo ya Biashara.
2. Huduma za fedha. HUDUMA ZA MAENDELEO YA BIASHARA ZA PASS
PASS inatoa huduma nyingi za maendeleo ya biashara kwa wateja kwa kuchangia gharama. Huduma hizo ni pamoja na;
- Upembuzi yakinifu.
- Kuandaa mipango ya biashara.
- Kujenga uwezo-mfano katika maeneo maalumu ya kitaalamu. Kuwaunganisha wakulima katika vikundi ambavyo vinaweza kutumika k**a vikundi maalumu kwa ajili ya kilimo cha mkataba, kusambaza pembejeo kwamkopo, kufanya mazungumzo ya bei na kutoa ushauri.
- Utafutaji na uunganishaji masoko. HUDUMA YA FEDHA
PASS itawasaidia watu na makampuni yanayostahili kupata mkopo kwa ajili ya uwekezaji wenye faida kupitia Tathmini ya maandiko ya kuombea mkopo kulingana na masharti ya benki husika na kulionganishwa na benki hizo: CRDB, NMB, EXIM,TIB,FBME,KCBL,BOA,ABC, AKIBA COMMERCIAL BANK, n.k. Dhamana ya mkopo ambayo inatolewa kwa benki zenye mikataba ya kushirikiana na PASS ili kujazia upungufu wa dhamana ya mteja. NANI ANAYEWEZA KUOMBA HUDUMA ZA PASS? Mtu binafsi yeyote, Vikundi, Chama au kampuni inaweza kutumia huduma za PASS haswa:
- Wajasiriamali binafsi - ambao ni watu binafsi, vyama au kampuni zinazoshughulika na sekta ya kilimo.
- Wajasiriamali binafsi - ambao wana dira na wanafanya biashara katika hali ya ufanisi na kibiashiara.
- Wajasiriamali binafsi - watakaoshirikiana na PASS na Benki washirika na kuwakilisha nyaraka zinazotakiwa na ambao wanaweza kufikia angalau vigezo vya msingi kwa ajili ya ukopaji. Kipaumbele kitatolewa kwa wateja wenye motekeo makubwa katika mwendelezo wa mnyororo wa thamani wa bidha za kilimo hususani katika mazao ya chakula, biashara na mazao ya kusafirishwa nje ya nchi.