Wakala Forum

Wakala Forum Jukwaa huru la mawakala wa huduma za kifedha Tanzania.

08/03/2026
The Earth is happy when women are happy.Happy international women’s day, Family!🥳
08/03/2025

The Earth is happy when women are happy.
Happy international women’s day, Family!🥳

Anatuandikia wakala: Alikuja jamaa mmoja smart hivi, muonekano wa kiboss. Aka-pack IST yake mbele ya ofisi na kuja kupat...
06/02/2025

Anatuandikia wakala: Alikuja jamaa mmoja smart hivi, muonekano wa kiboss. Aka-pack IST yake mbele ya ofisi na kuja kupata huduma ya kutoa pesa kiasi cha TZS.500,000/=

Alinichangamkia na kunifanya rafiki ndani ya muda mfupi. “Vipi naweza kutoa 500k mrembo?” Nikamjibu ndiyo. Akaanza kusifia ofisi yangu kuwa ni nzuri sana, nikamjibu Ahsante.

Kweli akatoa ile 500,000/= nikamhesabia nikampa. Punde akaja mtu mwingine nae akasema anatoa 200,000/=. Hisia zinaniambia walikuwa pamoja. Alikuja kuchukua attention yangu.

Huyu wa 200k akani-keep busy kidogo, wakati naendelea nae, huyu mwingine akaniambia naomba simu yako nikuandikie namba yangu ya simu uje umuulize Boss wako kuhusu fundi aliyetengeneza hapa nina shida nae.

Ak**aliza akaondoka. Huyu mwingine nae akaondoka. Baada ya k**a dakika 20 hivi nikaona sms Boss wangu(Muajiri wangu) akinipa maelekezo ya kutuma pesa kwenye namba fulani. Nikasema sawa, nikatuma.

Mara ya kwanza nilipewa maelekezo ya kutuma TZS400,000/=. Dakika moja tena akasema nitumie TZS600,000/= jumla iwe milion moja -Nikatuma. Akaniuliza kwenye mtandao mwingine kuna kiasi gani? Nikamwambia akasema tuma. Zoezi zima linaisha nilikuwa nimeshatuma TZS3,000,000/=.

Nilipokuja kushtuka ni pale aliponiuliza Bank fulani ina shilingi ngapi? Ndipo nikashangaa inamaana boss hajui kuwa hatuna hii huduma? Kuangalia Namba ya simu sio yake. Kumbe tapeli aliandika namba yake akafuta ya Boss muda ule nipo busy na mteja wa 200,000.

MBINU ALIYOTUMIA TAPELI:
1. Kujenga urafiki na mazoea
2. Alitoa hela halisi ili kumtoa hofu
3. Aliangalia sehemu ya SMS na kujua jina la Boss wake.
3. Ali-fake conversations za mwisho za Mfanyakazi na Boss wake.

USHAURI:
•SMS sio lugha ya kibiashara, Piga simu boss wako atoe maelekezo kwa mdomo na ujiridhishe pasi na shakakuwa hayupo sehemu hatarishi akiwa na akili timamu (Beyond reasonable doubt, with sound mind).

•Usimpe mtu ashike simu yako, namba mwambie akutajie uandike.

•Mambo ni mawili: asubiri/awe mpole uhudumie wateja au aondoke kwa amani.

Graphics: jordan Mallya
Caption: Hemedy, Esq.
06 February, 2025. Dar es salaam.

K**a ulikuwa unatafuta njia rahisi, salama, na yenye faida kubwa ya kukuza pesa zako,   kupitia M-Wekeza ni suluhisho bo...
01/02/2025

K**a ulikuwa unatafuta njia rahisi, salama, na yenye faida kubwa ya kukuza pesa zako, kupitia M-Wekeza ni suluhisho bora kwako!

Sasa unaweza kuwekeza moja kwa moja kutoka kwenye M-Pesa na kupata faida ya hadi 13% kwa mwaka BILA KUKATWA KODI! 4

Kwa Nini Uwekeze na M-Wekeza?

✅Faida Kubwa - Mpaka 13% kwa Mwaka. Pesa zako zinafanya kazi kwa ajili yako, huku zikiingiza riba nzuri inayokusaidia kukuza akiba na kufikia malengo yako ya kifedha haraka.

✅Hakuna Makato ya Kodi - Faida Yako ni Yako!
Tofauti na aina nyingine za uwekezaji ambapo faida inakatwa kodi, M-Wekeza haina makato ya kodi. Hivyo unapata faida yote bila kupunguza thamani ya uwekezaji wako.

✅Unaanza na Kiasi Kidogo - Kuanzia TZS 10,000 Tu.
Huhitaji kuwa na mtaji mkubwa ili kuanza kuwekeza. M-Wekeza inakupa nafasi ya kuanza na hata kiasi kidogo unachopata kwenye matumizi yako ya kila siku.

✅Uwekezaji Bila Usumbufu - Hakuna Makaratasi, Hakuna Safari za Benki! -
Kila kitu kinafanyika moja kwa moja kwenye simu yako kupitia M-Pesa, ukiwa mahali popote na wakati wowote - hakuna usumbufu wa kujaza fomu au kutembelea matawi ya benki.

✅ Fedha Zako Ziko Salama na Zinapatikana Wakati Wowote.
M-Wekeza inasimamiwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Tanzania (CMSA), hivyo pesa zako ziko salama.

✅Zaidi ya hayo, unaweza kutoa fedha zako wakati wowote kupitia M-Pesa bila kusubiri siku kadhaa k**a kwenye uwekezaji mwingine.

✅Inapatikana Kwenye Simu Yoyote - Hata Bila Smartphone!
Haijalishi unatumia smartphone au simu ya kawaida, unaweza kuwekeza kirahisi kwa kupiga 15000 # kisha kuchagua M-WEKEZA.

Graphics:Jordan Mallya
Caption : Hemedy, Esq.
Dar es salaam, Tanzania.
31 January 2025, 13:00 hrs

Siku ya jana tarehe 26.11.2024 TiGo Tanzania inayomilikiwa na Honora Tanzania Public Limited Company iliyotoa huduma kwa...
27/11/2024

Siku ya jana tarehe 26.11.2024 TiGo Tanzania inayomilikiwa na Honora Tanzania Public Limited Company iliyotoa huduma kwa miaka 30 ilifanya mabadiliko ya jina la “Brand” yao kutoka Tigo Tanzania na sasa itaitwa Yas Tanzania huku wakibadilisha jina la bidhaa yao “TIGOPESA” na sasa itaitwa Mixx by Yas.

Ikumbukwe kuwa hii si mara ya kwanza Kampuni hiyo kufanya maboresho kwenye huduma zao ikiwemo majina ya huduma zao. Mwaka 1994 baada ya kuanzishwa kwa huduma zake mwaka 1993 walianza kwa jina la MOBITEL jina lililotumika mpaka miaka ya 2000 na kubadilishwa kuwa BUZZ kisha mwaka 2006 kubadilishwa kwa mara ya tatu na kuwa TIGO Tanzania jina lililotumika mpaka hapo jana 2024 na kubadilishwa kuwa YAS TANZANIA kwa mara nne.

Huduma za Tigo na Zantel(YAS TANZANIA) sasa zinaenda kuunganisha (kwa kutumia hilo moja YAS) jumla ya nchi 5 ikiwemo Tanzania, Comoro, Senegal, Madagascar pamoja na Togo.

Kubadilishwa kwa majina kunachangiwa na sababu nyingi ikiwemo maboresho na malengo ya utoaji huduma, kubadilika shareholders na mikakati mipya ya kufikia huduma zaidi.

Ndugu wakala, airtel   wameendelea kuboresha huduma zao ambapo kwa sasa mtumiaji wa Lipa namba ya airtel hatokatwa tena ...
31/10/2024

Ndugu wakala, airtel wameendelea kuboresha huduma zao ambapo kwa sasa mtumiaji wa Lipa namba ya airtel hatokatwa tena tozo wala ada ya muamala tofauti na ilivyokuwa mwanzo.

Ni maboresho mazuri yaliyofanywa na Mtandao wa airtel katika kuwarahisishia wafanyabiashara na watumiaji wote wa lipa namba za airtel.

Ili kuweza kuingia kwenye menu ya kutoa pesa moja kwa moja kwa urahisi piga *150*60*06 # kisha endelea na hatua zinazofuata.

MAWAKALA NAWAKUMBUSHA JINSI YA KUTOA PESA KWA WAKALA MKUU⛽️ HALOTEL1️⃣ Piga *150*88 # then OK2️⃣ Chagua 7. Kutoa3️⃣ Chag...
16/10/2024

MAWAKALA NAWAKUMBUSHA JINSI YA KUTOA PESA KWA WAKALA MKUU

⛽️ HALOTEL
1️⃣ Piga *150*88 # then OK
2️⃣ Chagua 7. Kutoa
3️⃣ Chagua 1. Wakala Mkuu
4️⃣ Ingiza namba ya Tili ya Wakala Mkuu
5️⃣ Weka Kiasi
6️⃣ Ingiza namba ya siri
7️⃣ Thibitisha

⛽️ AIRTEL
1️⃣ Piga *150*60 # then OK
2️⃣ Chagua 1. Weka Pesa
3️⃣ Chagua 2. Weka kwa Wakala
4️⃣ Ingiza namba ya Simu ya Wakala Mkuu
5️⃣ Ingiza Kiasi
6️⃣ Ingiza namba ya siri
7️⃣ Thibitisha

⛽️ TIGO
1️⃣ Piga *150*01 # then OK
2️⃣ Chagua 5. Wakala kutoa Pesa
3️⃣ Chagua 2. Wakala kutoa Pesa kwa Wakala Mkuu
4️⃣ Ingiza namba ya Simu ya Wakala Mkuu
5️⃣ Weka Kiasi
6️⃣ Ingiza namba ya siri
7️⃣ Thibitisha

⛽️ VODACOM
_Ili uweze kutoa hela kwa Wakala Mkuu. Kwanza kabisa hakikisha fedha ipo kwenye Akaunti ya Mtaji✅. K**a ilikuwa kwenye Akaunti ya Kazi ihamishie kwenye Akaunti ya Mtaji. Baada ya hapo fuata hatua zifuatazo:_

1️⃣ Piga *150*00 # then OK
2️⃣ Chagua 5. Store Mgt
3️⃣ Chagua 2. Chukua Pesa
4️⃣ Weka namba ya Wakala Mkuu
5️⃣ Weka Kiasi
6️⃣ Weka Utambulisho wa Msaidizi
7️⃣ Weka Namba ya Siri
8️⃣ Bonyeza 1. Kuthibitisha

•Imekuwa ni kawaida kwa baadhi ya wateja kuondoka haraka baada ya kupatiwa huduma kwa wakala jambo ambalo siyo salama kw...
13/08/2024

•Imekuwa ni kawaida kwa baadhi ya wateja kuondoka haraka baada ya kupatiwa huduma kwa wakala jambo ambalo siyo salama kwa upande wa wakala na upande wa mteja.

•Ndugu wakala, hakikisha mteja wako anaona na kuthibitisha muamala uliomfanyia ili kuepuka kurudi baadae na malalamiko ya kwamba hajaona muamala.

•Pia hakikisha mteja wako anahesabu fedha vizuri na kujiridhisha pasi na shaka kabla ya kuondoka ofisini kwako. Hii itaepusha mkanganyiko endapo ataenda kuhesabia mbali na eneo la ofisi na kisha kukuta fedha ni pungufu.

•Slide namba mbili ni wakala mwenzetu ameamua kuweka bango la tangazo aliwasihi wateja wake wawe makini pindi wanapopata huduma kutoka kwake ikiwemo kuthibitisha muamala au kuhesabu fedha kabla ya kuondoka.

Ndugu wakala endelea kufuatilia kurasa zetu kwa mengi zaidi ya kujifunza.

Ndugu wakala, Imewahi kukutokea mteja amekuja ofisini kwako akataka kutoa kiasi cha fedha bila kutaja ni kiasi gani hali...
09/08/2024

Ndugu wakala, Imewahi kukutokea mteja amekuja ofisini kwako akataka kutoa kiasi cha fedha bila kutaja ni kiasi gani halisi anatoa na wewe bila kuuliza ukamruhusu atoe? Kisha akatoa pesa kubwa kuliko kiasi cha cash ulichonacho? Huwa unafanyaje?😁.

Sasa fanya hivi:👇
1. Muda wowote hakikisha unajua kiasi cha fedha ulichonacho kuanzia Floats za laini zote na kiasi cha Cash.

2. Mteja yeyote anapofika ofisini kwako na kuomba kutoa kiasi cha fedha HAKIKISHA UNAMUULIZA ANATOA KIASI GANI. Lengo ni kujua k**a cash yako inamtosha.

3. Huwa inatokea mara chache kwa baadhi ya wateja akikuta wateja ni wengi haulizi, yeye anatoa tu. Sasa ikitokea kesi k**a hii usipaniki, tumia busara. Mpe kiti akae dakika chache kisha kabadilishe cash au k**a una jirani anaweza kukupa kisha mkaendelea na biashara.

Hivi ndivyo huwa tunafanya sisi mawakala😁.
Tunawatakia jioni njema na weekend njema🫶🏻

Zaidi ya asilimia 60 ya Watanzania wote wanategemea kilimo k**a sehemu ya ajira. Tunapenda kuungana nao katika kusherehe...
08/08/2024

Zaidi ya asilimia 60 ya Watanzania wote wanategemea kilimo k**a sehemu ya ajira. Tunapenda kuungana nao katika kusherehekea siku yao hii maalumu.

Nyuso za watumiaji wa mtandao wa Tigo Tanzania  zimeshamiri furaha na tabasamu lisiloisha  baada ya Mtandao huo kutambul...
16/05/2024

Nyuso za watumiaji wa mtandao wa Tigo Tanzania zimeshamiri furaha na tabasamu lisiloisha baada ya Mtandao huo kutambulisha Aplikesheni yake mpya “SUPER APP” yenye muonekano mpya na ulioboreshwa zaidi ya hapo awali.

Kwenye muonekano huo mpya, utakutana na features mpya zitakazokufanya uendelee kupenda kutumia huduma za Tigo.

BAADHI YA FEATURES HIZO NI K**A ZIFUATAZO:

1. Unaweza kuwa na akaunti zaidi ya moja kwenye App moja(Linked account).
2. ⁠Sasa unaweza kutuma pesa kwa namba zaidi ya moja kwa wakati mmoja/Mkupuo(Send to Many).
3. ⁠Unaweza kuangalia Wakala aliyepo karibu nawe ili uweze kupata huduma za Tigopesa(Agents and shops).
4. ⁠Sasa unaweza kubadilisha muonekano(Theme) kutoka nyeupe na Nyeusi(Theme Selection).
5. ⁠Utaweza kupata huduma ya customer care ndani ya Tigopesa App. Huduma hii itatolewa kwa:
a. Contact us
b.FAQs
c. Tutorials for Tigo Pesa.

6. Unaweza kutuma pesa kwenda Bank moja kwa moja na kwa urahisi zaidi.
7. Unaweza kupata risiti ya muamala wako iliyoboreshwa zaidi.
8. ⁠Unaweza kuandika maelezo/Maelekezo ya muamala unaofanya.
9. ⁠Kuna ofa ya GB1 pindi utakapo-download App ya tigopesa😜.
10. ⁠Ofa nyingi za mara kwa mara kadri unavyotumia.

Ndugu Wakala, tunakutakia kazi njema na tunakuhimiza kutumia TigoPesa Super App.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wakala Forum posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share