09/05/2026
Katika ujumuishaji wananchi kiuchumi, Taasisi yetu ya CRDB Bank Foundation imetoa nafasi ya pekee kwa wanafunzi na wahitimu wa ndani ya miaka mitano iliyopita kubadili mawazo yao bunifu kuwa biashara halisi kupitia Mradi wetu wa IMBEJU - UDSM Startup Challenge 2026 tunaoutekeleza tukishirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mradi huu unalenga kubadili ripoti za utafiti na mawazo ya kijasiriamali kutoka chuoni hapo kuwa suluhu ya uhakika wa changamoto zinazoikabili jamii na taifa letu kwa ujumla.
Tukishirikiana na wabia wa kimkakati, tunaamini Programu yetu ya Imbeju itawafikia walengwa wengi hasa vijana na wanawake kote nchini, mjini na vijijini.