CRDB Bank Foundation

CRDB Bank Foundation Dira yetu ni kuboresha maisha ya watu wetu na kukuza uchumi

09/05/2026

Katika ujumuishaji wananchi kiuchumi, Taasisi yetu ya CRDB Bank Foundation imetoa nafasi ya pekee kwa wanafunzi na wahitimu wa ndani ya miaka mitano iliyopita kubadili mawazo yao bunifu kuwa biashara halisi kupitia Mradi wetu wa IMBEJU - UDSM Startup Challenge 2026 tunaoutekeleza tukishirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mradi huu unalenga kubadili ripoti za utafiti na mawazo ya kijasiriamali kutoka chuoni hapo kuwa suluhu ya uhakika wa changamoto zinazoikabili jamii na taifa letu kwa ujumla.

Tukishirikiana na wabia wa kimkakati, tunaamini Programu yetu ya Imbeju itawafikia walengwa wengi hasa vijana na wanawake kote nchini, mjini na vijijini.


25/04/2026

Siku ya Mwanamke Ilemela - Mwanza.

Elimu ya Fedha, Mafunzo ya Ujasiriamali na Uwezeshaji.


12/03/2026

Tarehe ya leo inaturudisha kwenye kumbukumbu ya uzinduzi wa CRDB Bank Foundation.

Leo ni miaka mitatu tangu tulipoanza safari ya kuwawezesha vijana na wanawake wajasiriamali katika jamii. Tumeshuhudia mawazo yakigeuka kuwa fursa na ndoto zikigeuka kuwa mafanikio.

Tunajivunia miaka mitatu ya kuwezesha jamii tukishirikiana na serikali na wadau mbalimbali katika safari hii yenye tumaini jipya.


08/03/2026

Tunapoadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, CRDB Bank Foundation tunajivunia kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko ya kweli kwa kuwawezesha wanawake nchini.

Kupitia programu yetu mama ya Imbeju, tumeendelea kuwasha taa ya matumaini kwa maelfu ya wanawake kwa kuwapatia elimu ya fedha na ujasiriamali, kuwawezesha kukuza biashara zao na kufikia masoko ya ndani na nje ya nchi. Haya si mafanikio ya kawaida bali ni safari ya kujenga ustawi wa familia, jamii na taifa kwa ujumla.

Nyuma ya mafanikio haya kuna uongozi thabiti wa mwanamke shupavu mwenye maono makubwa. Usikose leo saa 3:00 usiku kupitia UTV (Azam) tukipata fursa ya kusikia safari ya uongozi na mafunzo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Bi TullyEsther Mwambapa.

Karibu ujifunze, uhamasike na uamini kuwa kila mwanamke ana uwezo wa kuleta mabadiliko.



04/03/2026

Sikiliza moja ya vijana wetu akielezea alichojifunza jana kupitia Programu ya Ajira YE2 kwa kushirikiana na GIZ, uthibitisho wa jitihada zetu za kubadilisha maisha ya Vijana nchini.


27/02/2026

Mrembo Naturals ni mfano hai wa biashara changa inayoongozwa na vijana wanaojali mazingira na mustakabali wa dunia. Kupitia programu ya IMBEJU, wamepata elimu ya fedha, mafunzo ya ujasiriamali na mitaji nafuu iliyowawezesha kukuza biashara yao kwa kasi na ufanisi zaidi huku wakiendelea kulinda mazingira.

Na wewe unaweza kuwa hadithi inayofuata ya mafanikio. Chukua hatua leo kwa kuwasilisha maombi yako kushiriki katika programu ya Go Green na IMBEJU kupitia apply.fursahub.com.

Hii ni fursa ya kipekee kwa vijana wanaotaka kukuza biashara zao, kuongeza thamani ya bidhaa na huduma zao, na kujenga biashara endelevu zenye tija kwa jamii na mazingira.


17/02/2026

Usisubiri Kesho

Kuna vijana tayari wameanza kutuma maombi yao.

Wewe je?
Fursa k**a hizi huja mara chache, fuatilia video hii kufahamu jinsi ya kuwasilisha maombi.


Address

PLOT No. 25, 26 Ali Hassan Mwinyi Road
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when CRDB Bank Foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to CRDB Bank Foundation:

Share