Avis Channel

Avis Channel Avischanneltv

24/06/2025

DAR: Siku moja kabla ya mchezo dhidi ya kwenye Uwanja wa Mkapa, Uongozi wa haujatuma wawakilishi katika Mkutano uliohusisha Wanahabari ambao ni maalum kwa ajili ya kuzungumzia mtanange huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kufanyika kesho Jumatano Juni 25, 2025

Taratibu za Ligi hiyo ni kuwa siku moja kabla ya mchezo, timu husika zinatakiwa kutuma Kocha na Mchezaji kuzungumza na Wanahabari kuhusu mchezo unaofuata ambapo ni ratiba pia inayofuatwa na Azam TV ambao wanahusika kurusha matangazo ya Ligi

Soma https://jamii.app/SimbaMkutanoni

24/06/2025

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Kheri James kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kuchukua nafasi ya Peter Serukamba

24/06/2025

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uteuzi alioufanya leo June 23 2025, amemteua Mkuu wa zamani wa Jeshi la Polisi Tanzania Balozi Simon Nyankoro Sirro kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Balozi Simon Sirro ni miongoni mwa Wakuu wapya wa Mikoa watano ambao wameteuliwa leo June 23 2025 ambapo wengine ni Kheri Dennis James aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Iringa, Mboni Mhita aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga, Beno Malisa aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Mbeya na Jabir Makame aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe.

24/06/2025
24/06/2025

Kuelekea mchezo wa Kariakoo dabi Jumatano ya Juni 25,2025 (kesho) Kikanuni Simba na Yanga zilitakiwa kufanya mkutano na waandishi wa habari hii leo ili kuelezea maandalizi na mambo mengine kuhusu mechi yao

Wenyeji wa mchezo Yanga SC wao wamefika na kufanya mazungumzo lakini Katika hali isiyo ya kawaida Simba SC hawajafika eneo ambalo mkutano ulipangwa kufanyika na jitihada za kuwatafuta zimegonga mwamba hivyo mkutano huo umeahirishwa ili kuendelea na ratiba zingine

“Simba walitakiwa kuwa hapa saa 5:30 asubuhi lakini hawajafika , kwa bahati mbaya hata kwenye simu hawapatikani na sisi hatuwezi kukaa hapa hadi saa 10 kwa sababu ratiba zingine zinatakiwa kuendelea” amesema Afisa habari wa Bodi ya Ligi Karim Boimanda wakati anaahirisha mkutano huo

23/06/2025

BODI ya Ligi kuu ya soka Tanzania bara TPLB imetangaza maofisa wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo kwenye Ligi Kuu bara kati ya wenyeji Young Africans Sc dhidi ya Simba Sc ambapo mchezo huo namba 184 utachezeshwa na waamuzi kutoka nchini Misri.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF, Mwamuzi wa kati atakuwa Amin Mohamed Amin Omar kutoka Misri akisaidiwa na Mahmoud Ahmed Abo El Regal k**a Mwamuzi msaidizi namba 1 na Samir Gamal Saad Mohamed ambaye atakuwa msaidizi namba 2.

Ahmed Mahrous naye kutoka Misri atakuwa ‘4th Official' naye kutoka Misri huku Kamishna wa mchezo huo utakaopigwa Juni 25, 2025 saa 11:00 jioni katika dimba la Benjamin Mkapa akitarajiwa kuwa Salim Omary Singano.

23/06/2025

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara imetangaza kuwa Mchezo wa Ligi hiyo wa kukamilisha Msimu wa 2024/25 ambao pia utaamua timu itakayotwaa ubingwa kati ya Yanga dhidi ya Simba (Kariakoo Derby) utachezeshwa na Waamuzi kutoka Nchini Misri

Mwamuzi wa kati atakuwa Amin Mohamed Amin Omar, Msaidizi Namba Moja ni Mahmoud Ahmed Abo El Regal, Msaidizi Namba Mbili ni Samir Gamal Saad Mohamed na Mwamuzi wa Akiba ni Ahmed Mahrous Elghandour

Kamishna wa Mchezo ni Salim Omary Singano kutoka Tanga wakati Mkaguzi wa Waamuzi ni Alli Mohamed kutoka Somalia

Pia, Catherine Chammy kutoka N-Card amesema “Kadi zilezile ambazo zilitumika Juni 15, 2025 kabla ya mechi kuahirishwa na kupangiwa siku nyingine ambayo ni Juni 25, 2025, zitatumika tena.”

Soma https://jamii.app/DabiYaKariakoo

03/01/2025

Msafara wa wajumbe 37 wa klabu ya TP Mazembe wakiwemo wachezaji 24 ambao wameondoka Lubumbashi na Air Tanzania kuja Dar-es-Salaam kwa ajili ya mchezo wao nne wa hatua ya makundi dhidi ya Yanga Sc utakaopigwa siku ya Jumamosi.

MAKIPA
1. Aliou FATY
2. Ibrahim MOUNKORO
3. Siadi BAGGIO

MABEKI
4. Magloire NTAMBWE
5. Johnson ATIBU
6. Mortalla MBAYE
7. Josué MUNGWENGI
8. Abdallah RAJABU
9. Elie MADINDA
10. Ernest LUZOLO
11. Ibrahima KEITA
12. Madou ZON

VIUNGO
13. Boaz NGALAMULUME
14. Patient MWAMBA
15. Jean DIOUF
16. Bank's MBUNGU
17. Sozé ZEMANGA
18. Basile KONGA

WASHAMBULIAJI
19. Dylan LUMBU
20. Oscar KABWIT
21. Gloire MUJAYA
22. Cheikh FOFANA
23. Faveurdi BONGELI
24. Satala ASSANI

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

+255689519563

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Avis Channel posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share