09/10/2024
NILIMDHANIA KAHANA KUMBE BIKRA
MTUNZI: SINGANO JR
SEASON 14
WhatsApp: 0687151346.
SEHEMU YA 391.
Baada ya Jeremy kutoka Kizwe alijikuta akilia kilio kisichokuwa cha kawaida , alikuwa akijitahidi tu kuwa jasiri mbele ya Raisi Jeremy lakini ukweli alikuwa akiogopa sana , hakuamini ndio hivyo anakwenda kufa , tena mtu ambaye anakwenda kumuua ni mume wake ambaye ameoana nae kwa miaka mingi.
“Kumbe mwenzangu ulikuwa mke wa raisi , ukashindwa kunipasha habari?”Aliongea Lekcha bila wasiwasi.
“Haijalishi kuwa mke wa raisi kwasasa kwani haina maana , mimi ni mwanamke ambaye nina laana ndio maana mume wangu mwenyewe ananiua”Aliongea huku akiwa ni mwenye huzuni.
“Kuna kitu nimeona katika maongezi yako, kauli yako ya mwisho inaonyesha haikuwa na ukweli wowote , si kweli ?”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha kauli yako ya kumuua sijui nani , haina ukweli wowote na umeongea ili kumpandisha jazba”
“Umejuaje?”
“Kwa muonekano wako , unaweza kuwa mkatili lakini naamini pia ulikuwa ukiheshimu cheo chako , siamini k**a wewe mwenyewe ndio ulitekeleza kifo cha huyo mwanamke , kuna uwezekano aliefanya hivyo ni mtu mwingine”Aliongea Lekcha na kumfanya Kizwe kupata nuru kidogo ya furaha.
“Inakuwaje mtu k**a wewe ukanielewa sana kuliko hata mume wangu , ni kweli sijamuua , ijapokuwa nilikuwa na chuki sana zidi yake , lakini kuna watu pia waliokuwa wakimchukia kuliko mimi, nilichokifanya nikuongezea kachumbari tu, mtu k**a wewe unaeonekana kunijali na kunielewa tunakutana nikiwa kwenye hatua za mwisho za kifo changu”
“Hehe haina haja tena ya kulalamika na kutoa hayo machozi , wote tunakwenda kufa .. ila sio mbaya ni kheri nakufa sasa nikiwa na mke wa raisi kuliko ningefia kule majalalani”Aliongea huku akiwa haeleweki ni hisia gani alizokuwa nazo kwenye moyo wake.
“Kuna namna ya wewe kuishi , nishaifikiria tokea tunaletwa hapa..”Aliongea Kizwe na kumshangaza Lekcha.
“Unasemaje , usiniambie k**a kuna namna ya kumfanya mheshimiwa kubadili mawazo na kutuacha hai wote”
“Simaanishi mimi, namaanisha kuna namna ya wewe kuishi hawezi kuniacha hai kwani ananiona k**a adui kwenye uongozi wake , kwa upande wako wewe huna thamani kwake akuue au asikuue ila k**a utakuwa na kitu cha kumbadili mawazo atakuacha hai”
“Kwahio ni kipi naweza kufanya ili kumpa sababu ya kuniacha hai?”Aliuliza na Kizwe alimpa ishara ya kumsogelea na kisha akamnong’oneza.
“Una uhakika na jambo hilo , hiki kitu ni hatari k**a kitafahamika?”
“Ndio, unachotakiwa ni kuongea k**a nilivyokueleza na atakuamini , kadri utakavyokuwa msiri atakuwa hana sababu ya kukuua na atakuacha hai na huenda akakupa ulinzi pia”
“Kwanini unaniambia haya mimi , ungemwambia wewe huenda angekuacha hai?”
“Hawezi kuniacha hai hata nikimuambia , nilijua muda mrefu tokea tunak**atwa kule Tanzania na kutuleta kwa ndege ya jeshi , siku zote alikuwa akitafuta namna ya kuachana na mimi na amepata nafasi hivyo haawezi kuipoteza”
“Lakini utakuwa na sababu ya kuniambia hivi pia ili kuniokoa na kifo?”Aliuliza Lekcha akiwa kwenye kuchanganyikiwa.
“Ndio sitaki kukulipa mabaya kwa yale ulionitendea , kwenye Maisha yangu niliishi Maisha ambayo sikuwahi kukosa pesa , lakini kitu kikubwa nilichokosa ni mapenzi ya dhati , siku mbili tulizokuwa pamoja nimeguswa sana na uwepo wako kwenye maisha yangu , Nakufa kabla ya kujua historia ya Maisha yako , lakini k**a utaishi naomba uniahidi kitu kimoja”
“Nipo tayari kukuahidi chochote?”Aliongea na kumfanya Kizwe atoe tabasamu la uchungu.
“Hakikisha unaishi Maisha yenye sababu kubwa , naamini kwa umri wako bado una nafasi ya kufanya makubwa , lakini jambo lingine nataka kukuona ukitimiza kitu ambacho ulisema ni tofauti na pesa”Aliongea na Lekcha kwa huzuni sana alitingisha kichwa chake kukubaliana nae.
Muda huo huo mlango wa chumba chao ulifunguliwa na watu wawili waliovalia makoti ya kimaabara wakiwa na vijitray vilivyojaa mabomba yenye vimiminika ndani yake kwa ajili ya kufanya kazi yao.
“Mwambieni mheshimiwa , huyu bwana hapa anasiri anataka kumweleza, toeni msisitizo kwamba siri hio itamfanya kumuacha hai na mtu atakaekufa siku ya leo atakuwa ni mimi pekee”Aliongea Kizwe na kisha alisimama haraka na kuchukua bomba lenye kimiminika na kisha akajichoma mwenyewe kwenye shingo akilenga mshipa mkubwa wa damu ,hata wale wataalamu wa maabara walishangazwa na kitendo chake , lakini walijikuta wakisimama wakimwangalia Kizwe akitapatapa na ndani ya dakika tano tu alikata moto na kunyoosha miguu huku macho akimkodolea Lekcha,
Lekcha alitolewa kwenye chumba mara baada ya taarifa kutolewa kwamba alikuwa na siri ya kumuelezea raisi Jeremy, baada ya kuburuzwa na mabodigadi alijikuta akigeuka nyuma na kumwangalia Kizwe aliekuwa chini hana uhai alijikuta moyo ukimuuma sana kwa mara ya kwanza kwenye Maisha yake , hakuamini k**a kweli mwanamke huyo aliemuokoa kule jijini Dar Es salaam ndio huyo amekufa kifo cha aina hio , alijihisi mkosaji na kujiambia huenda angemuacha tu ajiue kule kule kuliko kuuliwa na mume wake.
Dakika chache mbele Lekcha alipelekwa mpaka ofisini kwa Raisi Jeremhy na kishwa kutupwa chini na mabodigadi.
*******
Taarrifa iliotolewa na Makedoni ilimchanganya sana Roma na kujiuliza ni mtu gani anajaribu kumchokoza.
“Mfalle Pluto huna haja ya kunificha , tumekuwa marafiki kwa muda mrefu, niambie k**a kweli umehusika?”Aliongea Makedoni.
“Nieleze kwa kina nini kimetokea sijui chochote”
“Kwahio unasema sio wewe?”
“Sio mimi kwenye nini Makedoni hebu acha kuwa mwanasiasa”Aliongea Roma
“Mfalme hili swala mbona k**a ni la ajabu, nusu saa iliopita meli ya Marekani iliokuwa ikirudi kutoka kusini mwa bahari ya China imeharibiwa , ni kati ya meli zilizokuwa na mzozo na taifa la uchina katika mgogoro unaoendelea na Taiwan , sasa kubwa yake yenye uwezo wa kubeba ndege za kivita za Nimtz na wanajeshi elfu moja wanamaji ndio ilioharibiwa na mtu ambaye unafanana nae kwa asiliamia mia moja”Aliongea Makedoni.
“Mbaya Zaidi mfalme Pluto ni kwamba meli hio pamoja na wanajeshi na baadhi ya ndege zilizokuwemo vimeharibiwa ndani ya dakika moja tu na kuzama ndani ya bahari”Aliongea Makedoni..Roma alishanga
“Makedoni unamaanisha kwamba mtu aliehusika ana uwezo k**a wangu ?”
“Ndio mfalme Pluto ,ijapokuwa ni mara chache sana nimeshuhuduia ukitumia uwezo wako wote , lakini mtu aliefanya hivyo naweza kusema kwamba anakukaribia na amefanya k**a ilivyokuwa kawaida yako na tukikadiria , inaonekana ni k**a unapofikia hatua ya macho yako kuwa mekundu”Aliongea Makedoni
“Hebu subiri , si umesema unayo Vidio?”
“Vidio tunayo , meli hio imerekodi tukio kwa dakika kadhaa na nimeweza kuiiba kutoka shirika la kijasusi la Marekani na kuangalia ndio maana nikakupigia”
“Nitumie hio video niangalie mwenyewe”Aliongea Roma na Mekedoni alikata simu na kisha akamtumia wakati huo huo video hio.
Roma aliweza kuangalia kila kitu kupitia tarakishi yake , ni kweli kabisa kilionekana kivuli ambacho kinafanana kabisa k**a yeye , tena kikishuka kutoka angani na kilivyoshuka karibu na meli ile alifanya makusudi ya kuangalia Kamera na palepale ulitokea mlipuko mkubwa k**a wa bomu ambao hata Kamera zilishindwa kuonyesha kilichoendelea, lakini kitu kikubwa ambacho Kamera hizo zilifanikuwa kurekodi sura yake halisi, kilichomtofautisha ni mavazi tu basi.
Baada ya kumaliza tu kuangalia palepale simu yake tena iliunganishwa na ya Makedoni.
“Your majest Pluto that wasn’t you?”
“Mfalme sio wewe si ndio?”
“No”
“Then”(Kwahio)
“That was spacetime manipulation but that man is definitely not me I can’t explain why he look like me though”Aliongea Roma
“Hio ni mbinu ya umanipulishaji wa muda wa Anga , lakini huyo mtu hakika sio mimi siwezi kuelezea kwanini anafanana na mimi lakini”Alijitetea Roma .
“Inaweza kuwa ‘Clone’ lakini hilo haliwezekani, k**a kweli ni Clone inawezekana vipi mtu kuiba DNA zako bila ya wewe mwenyewe kufahamu? Lakini hata k**a iwe ni Clone haileti maana kuweza kuwa na uwezo wa kucheza na Muda wa anga”
“Hakuna mtu anaeweza kunifanyia Clone kwasababu mwili wangu tayari ulishamulikwa na Devine light, hata mimi mwenyewe nishawahi kujiuliza k**a mtu anaweza kuiba damu yangu na kutengeneza siraha ya kibailoia , lakini tafiti zilizofanywa zilibainisha hilo haliwezi kufanikiwa, kwasababu lazima waweze kupata damu yangu ikiwa ya moto kabisa na isigusane na hewa, lakini pia inawezekanaje mtu kuiba damu yangu nisijue?”
“Kweli kabisa mtu kuiba damu yako na wewe mwenyewe usifahamu , nadhani ni jambo ambalo haliwezekani kabisa”Alijibu Makedoni upande wa pili.
“Hilo sio muhimu kwa sasa k**a wataweza kutengeneza kopi ya mwili wangu haitakuwa na uwezo wa kuwa na nguvu za kuchezea kanuni za anga na kuwa tishio , kwa jinsi ninavyomuona kwenye hii Video anaonekana kuwa na uwezo wake binafsi”Aliongea Roma
“Mfalme Pluto lazima tufanye jambo , ni kweli kabisa mtu hiyo ana nguvu k**a za kwako lakini jambo kubwa ni kwamba haheshimu kabisa The Gods Treaty , ameharibu meli yote ya kivita lakini pia anafanana na wewe , k**a serikali ya kimarekani hawataweza kumtambua inamaanisha kwamba…”
“Makosa yake yote yatasukumiwa kwangu, kwasababu sitakuwa na ushahidi wa kutosha wa kujitetea , lakini pia huyu mtu sijui ni nani na kwanini kafanya hivyo”
“Ni kweli mfalme Pluto , serikali ya Marekani imeomba pia idara yetu kufanya uchunguzi , ni wenye hasira kwasasa kwani wanaamini umeanza kuvunja sheri za kimkataba ndani ya The Gods Treaty na kuegamia upande wa China, siku mbili zilizopita serikali ya Marekani na serikali ya kichina iliingia kwenye makubaliano ambayo Marekani ilibidi kuondoa meli na wanajeshi wake wote waliokaribu na mipaka ya China kutokana na mzozo unaondelea kati ya Taiwani na China , jambo ambalo Marekani ilitekeleza mara moja na meli ilioharibika ilikuwa kwenye safari ya kurudi Marekani na Zaidi ya wanajeshi wao elfu moja makomandoo wamekufa, Mpaka sasa wanaamini moja kwa mja unatumia uwezo wako kuiinua China kijeshi”
“Achana na maswala ya siasa Makedoni , kwasasa mtu huyu kavunja sheria za Gods Treaty mchana kweupe , ni lazima miungu mingine itachukua hatua zidi yangu , Makedoni nadhani mlifanye swala hili siri kwanza maana ninaweza kushambuliwa muda wowote , mbaya Zaidi ametumia mbunu zangu zote zilizo zoeleka hivyo hakuna namna ya kujitetea”
“Mfalme Pluto unamaanisha serikali ya kimarekani inao uwezo wa kuamrisha miungu mingine kukushambulia , je wanaifahamu?”
“Haina haja ya kuwaomba , unajua Christen yupo Marekani na wote wanazo koneksheni za kujua ni nini kinaendelea kwenye dunia , ni Dhahiri mpaka sasa watakuwa na taarifa”
“Sawa nitajaribu kuangalia namna ya kuituliza hali”
“Utakuwa umenisaidia , hili ni swala kubwa mno na mimi mwenyewe nitalifanyia kazi , nitaondoka Tanzania kuelekea bahari ya kusini sasa hivi” Aliongea Roma na palepale simu yake ilikatika ,hakuwa hat ana haja ya kuaga kwani alipotea mara moja.
Unachotakiwa kutambua likija swala la ‘Space Time Manipulation’ kuharibu kitu cha Zaidi ya tani elfu moja ni k**a kukata kijiti tu na hicho ndio kilichofanyika kwa Meli ya kivita ya Kimarekani , mtu alieonekana akifanana na Hades alikuwa na ‘Spatial Powers’ ambazo anaweza kuchezea kanuni za anga kwa kutumia ‘Gravity’na kufanya anachotaka.
‘Quantam Mechanic’ na ‘General relativity’ inaelezea kwamba anga na muda ni vitu ambavyo havitofautiani katika utendaji wao na k**a vitakusanywa pamoja ndio hutengeneza Muda wa anga, kwahio Eistein mwenyewe anahusisha maswala yote ya kani mvutano na mengineyo ya kifizikia yanabebwa ndani ya Space na muda, Taasisi ya utafiti wa mambo ya anga ya Kimarekani ya NASA kwa kutumia kifaa chao cha NASAs Gravity Probe B waliweza kuthibitisha nadharia ya Eistein kwamba ni kweli anga na muda ni vitu vilivyoungana na vipo vinafanya kazi.
ITAENDELEA
NISAPOTI KWA KUSHARE ILI PAGE IKUE NA SIMULIZI ZIWE NYINGI