09/02/2018
Moja kati ya wafanyabiashara wakubwa mjini Moshi, Bwana Miraji Ali Kidundi almaarufu k**a CHAKITO, mmiliki wa mabasi makubwa ya kusafiria yanaoenda Dar , Arusha pamoja na vituo vya mafuto petroli, dizeli na mafuta ya taa, vinavyopatikana maeneo ya Moshi, Same na Lushoto akielezea uzuri wa Mwanga Community Bank na jinsi ilivyomtoa kutoka mfanyabiashara wa kawaida na mpaka sasa amekua moja kati ya wafanyabiashara wakubwa mjini humo, anaemiliki mabasi ya kusafiria, vituo vya mafuta, kumbi za sherehe pamoja na vituo vya utalii.
"Nimeanza kutumia benki yetu ya wananchi kwa muda mrefu sasa nina zaidi ya miaka kumi na nimeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa tangu nimeanza kufanya hizi biashara.Nilianza kukopa kuanzia milioni 4 za kitanzania na sasa ninaweza kukopa zaidi ya milioni 100. Mkopo wa sasa unafika hadi 400 milioni ambao ndio namalizia kuurejesha.Naipenda Benki yetu kwa sababu haina ubabaishaji kwenye utoaji wa mikopo, pia urahisi wa kufanya malipo ninapotaka kuagioza mzigo pesa zinatumwa kwa wakati kwenda kwa wasambazaji, makao makuu yapo kilimanjaro hvyo ni rahisi kufanya maamuzi. watu wasiangalie jina waangalie ni vitu gani, uaminifu na uwezo gani benki ilionao katika kihudumia wateja wake."
Pia aliongeza kwa kuwaasa wafanyabiashara wakubwa kuwekeza kwenye beni hii na kufurahia matunda mazuri ambayo na yeye yameweza kumfikisha alipo sasa.