24/10/2022
TAJIRIKA MAPEMA.
Nakusalimu.
Mimi ni KUMBUAEL KAAYA 0769160382
Naomba usome kuhusu kutajirika mapema.
Biashara za mtandaoni za tajirika mapema zimekua nyingi sana katika zama hizi za utandawazi. Wengi wanaathirika na huu uvumi kwa sababu ya tamaa ya kua Tajiri. Napenda kua Tajiri hata mimi ieleweke hivyo.
Tajirika mapema ni nini? Ni mpango unaoahidi kumfanya mtu kuwa tajiri sana kwa muda mfupi. Ipo mifano mingi sana ambayo hata wewe utakua unafahamu. Swali, je ulishawahi kusikia hao wanaotangaza hiyo mifumo ya kutajirika mapema wakisema wanafanya biashara gani mpaka wapate hizo faida?
Embu fikiri pamoja na mimi mtu anakwambia ukiweka laki moja unapata faida ya elfu 30 kwa wiki, ni biashara gani unafanya upate faida kwa wiki ambayo unatoa gharama zako zote na bado unatoa gawio la elfu 30 kwa wiki kwa mtaji wa laki moja. Taasisi ndogo za fedha zinakukopesha uwalipe riba ya asilimia 3 kwa mwezi, wakufuatilie, kukudai na maform mengi unajaza je hujawahi kujiuliza kwanini hawa matapeli k**a inalipa wasiende kukopa benki warudishe marejesho maana wakopeshaji wanataka riba ndogo tu asilimia 3 sio kubwa?
Nakushauri ukitaka kuwekeza pesa yako mahali hakikisha unapafahamu vizuri. Inakuaje mtu anakueleza habari za namna utapata faida unakubali kirahisi tu unaweka pesa bila hata kua na taarifa za kutosha.
Unachukua mtaji wote unawapa watu wakati mtu aliepewa Hekima nyingi sana na Mungu mfalme Suleimani kwenye Kitabu cha Mhubiri 11:2 Uwagawie sehemu watu saba, hata wanane; Maana hujui baa gani litakalokuwa juu ya nchi ameshakwambia usiweke mahali pamoja hujui baa gani litakuwepo hata k**a unapafahamu, wewe unampa mtu usiemjua tena pesa zote.
Watu wengi wanalia sana sasa hivi kila mahali wametapeliwa pesa zao, mara mtu anaenda kuchukua mkopo Benki ili awekeze inaliwa pesa unalipa mkopo miaka 10 utakua na afya ya akili kweli wewe? Tunasingizia michango mingi kanisani kumbe ni kwa sababu tumeshaibiwa huko na matapeli.
Katika elimu za muhimu sana nakusahuri uwe nazo ni elimu ya fedha na naomba ukiona pesa zako zinapotea kwa mwendo kasi kuliko zilivyokuja ujue tayari shida mahali.
Kabla ya kuwekeza tafuta elimu au kujua huo uwekezaji unafanyaje kazi. Kua makini na pesa zako. Ukiona unaingia kwenye uwekezaji ambao wewe binafsi hauna utaalamu wake tafuta ushauri na umuombe Mungu usizitegemee akili zako mwenyewe! Nitafute
Karibu.