Epak Capital

Epak Capital Our Goal is to Build a Fortress Investment Company That Creates 5X to 10X+ Investment Returns to Investors in Mid and Long Terms.

Kisasi bora zaidi ni kutolipiza kisasi kabisa. Pona, songa mbele na usiwe k**a wale waliokuumiza.
05/08/2024

Kisasi bora zaidi ni kutolipiza kisasi kabisa. Pona, songa mbele na usiwe k**a wale waliokuumiza.

Darasa la Bure la Tabia - Tabia Mama (Keystone Habits) na Tabia za PembezoniKuna tabia mama na tabia za pembezoni. Tabia...
25/07/2024

Darasa la Bure la Tabia - Tabia Mama (Keystone Habits) na Tabia za Pembezoni

Kuna tabia mama na tabia za pembezoni.

Tabia mama ni zile ambazo zina mizizi mirefu ama juu yake kuna tabia nyingine nyingi. Ama ni tabia zinazoathiri maeneo mbalimbali ya maisha ya mtu.

Tabia za pembezoni ni zile tabia ambazo ni matokeo ya tabia mama. Tabia ndogo ndogo ambazo madhara yake hayaendi mbali sana kwenye maisha ya mtu.

Mfano 1: Tabia ya kupigana/kufanya vurugu baada ya kunywa pombe
Mtu aliye na tabia ya kupigana baada ya kunywa pombe. Tabia mama ni pombe na tabia ya pembezoni ni kupigana baada ya kulewa. Mtu huyu akiacha kunywa pombe ataacha na tabia nyingine zote zinazokuja na ulevi.

Mfano wa Pili: Mtu mwenye tabia ya kukosa pesa(broke) muda mwingi. Hii ni tabia inayowaathiri watu wengi.

Tabia ya kuwa huna pesa ni matokeo ya tabia nyingine nyingi. Mfano tabia ya kutokuwa na bajeti, tabia ya kununua vitu bila kupanga, tabia ya kutokuweka akiba, tabia ya kutojali hali yako ya kifedha, tabia ya ulevi, tabia ya kuchepuka au kuwa na mahusiano mengi, na kadhalika.

Moja ya njia ya kukabiliana na tabia hii ya kukosa pesa ni kujenga tabia mpya ya kutumia bajeti. Hata hivyo kutokana na ukweli kuwa tabia haziwezi kufutika bali zinaweza kubadilishwa itabidi ufanye kazi ya ziada kubadilisha tabia hizi.

Suluhu ya hali k**a hii ni kujenga tabia mpya ya kuwa na mazungumzo na vikao vingi vya kina na watu wanaokusumbua ama washauri ili uweze kuelewa tatizo na kuweza kulitatua. Kunywa pombe au kuchepuka na pisi hakuwezi kuwa suluhu ya changamoto.

Mfano wa 3: Tabia ya kunywa pombe hadi kulewa kila unapokasirishwa ama unapokuwa na mawazo.

Hii ni tabia inayotokana na kukwepa kufikiri ama kutatua matatizo ama changamoto zinazomkabili mtu. Tabia hii ya kulewa badala ya kufikiri na kitafuta watu wanaoweza kukushauri ni tabia ya pembezoni.

Mfano ya 3: Tabia ya kuangalia sana simu ama vifaa vya kielektroniki.

Hii tabia ni tabia mama kwani inaathiri mambo mengi kwenye maisha ya mtu. Inaathiri afya ya macho, afya ya akili, huathiri mahusiano na watu wengine, huathiri ufanisi kazini au kwenye biashara na kadhalika.

Mtu akiweza kujenga tabia njema kwenye matumizi ya simu na vifaa vingine vya kielektroniki ataweza kuathiri maeneo mbalimbali ya maisha yake.

Jambo moja nimejifunza juu ya tabia kutoka kwenye kitabu cha The Power of Habit ni kuwa kila mtu anatakiwa kujua tabia gani kwenye maisha yake ni mama(Keystone Habits) na tabia gani ni matokeo ya tabia nyingine.

HADI KUFANIKIWA, UTAFELI MARA NYINGI - KUFELI NI ISHARA KUWA UNAJIFUNZA NA UNAJARIBU MAMBO MAPYA. Masomo 10 kutoka kweny...
25/07/2024

HADI KUFANIKIWA, UTAFELI MARA NYINGI - KUFELI NI ISHARA KUWA UNAJIFUNZA NA UNAJARIBU MAMBO MAPYA.

Masomo 10 kutoka kwenye kitabu, "Jinsi ya Kufeli Kwenye Karibu Kila Kitu na Bado Uibuke Mshindi: Hii ni K**a Simulizi ya Maisha Yangu" ("How to Fail at Almost Everything and Still Win Big: Kind of the Story of My Life") cha Scott Adams, ambaye anatufundisha namna inayotekelezeka ya kutumia kufeli kuelekea kwenye mafanikio.

1. Jali Kujenga Mifumo Zaidi ya Malengo(Systems Over Goals): Weka fokasi yako kwenye kujenga mifumo badala ya kuweka malengo. Mifumo ni michakato inayoendelea inayokuongezea uwezekano wa kufanikiwa, wakati malengo ni shabaha mahususi ambayo yanaweza kupelekea kutofurahisha yanapofikiwa.

2. Weka Kipaumbele Kwenye Jinsi Unavyojisikia na Nguvu Yako (Prioritize Your Energy): Tawala nguvu yako kuliko muda. Weka fokasi yako kwenye mambo na majukumu yanayokuongezea nguvu na achana na yale yanayokunyonya nguvu.

3. Jifunze Kutokana na kufeli(Learn From Failure): Kumbatia kufeli k**a fursa ya kujifunza. Kila kufeli huwa na masomo yanayoweza kukuongoza hadi kwenye mafanikio.

4. Jijengee Maarifa(Skill Stacking): Jiendeleze hadi uwe na seti za mbalimbali za maarifa. Kuunganisha maarifa ya kawaida katika maeneo mbalimbali kunaweza kukufanya uwe na thamani kubwa na mwenye mafanikio kuli kuwa na maarifa makubwa kwenye eneo moja pekee.

5. Kukiri(Affirmations): Tumia njia ya kukiri mambo chanya juu yako na yale unayoyataka ili kuprogramu akili yako kubwa kwaajili ya mafanikio. Kurudia kauli chanya kunaweza kukufanya ufokasi kwenye malengo yako.

6. Mfumo wa Maisha Unaojali Afya Njema(Healthy Lifestyle): Jenga mfumo wa maisha unaojali afya njema unaojumuisha kufanya mazoezi ya mara kwa mara, mlo kamili na kulala vya kutosha. Afya njema hukuwezesha kuwa na nguvu, ubunifu na uzalishaji.

7. Badililika na Hali na Mazingira (Adaptability): Kuwa tayari kubadilika na hali na mazingira, badilika namna unavyofanya mambo pale ambapo hupati matokeo. Kuwa mwepesi ni ufunguo wa kushinda vikwazo na kupata njia mpya za kufikia mafanikio.

8. Weka Mkazo Kwenye Miradi yako Binafsi (Focus on Personal Projects): Jishughulishe kwenye miradi yako binafsi ambayo inakuvutia na inayoendana na uimara wako. Miradi ambayo mtu anaipenda inaweza kupelekea kwenye fursa na mafanikio.

9. Kumbati Utofauti Wako(Embrace Your Weirdness): Tumia uwezo wako wa kipekee na mitazamo yako. Kuwa mkweli na halisi kunaweza kukutofautisha na kuvutia mafanikio.

10. Kuhusiana na watu na kujenga mahusiano (Networking and Relationships): Jenga na kuwa na mtandao imara wa mahusiano. Mahusiano yanaweza kukufungulia milango ya fursa mbalimbali na kukupatia msaada pale unapohitaji.

Masomo haya yanasisitiza umuhimu wa kuwa mstahimilivu, kuendelea kujifunza, na kuwa na mkakati wa kukua k**a mtu binafsi na mweledi.

Asante kwa kusoma na kushea 🙏🙏🙏

BINTI WA MAZIWA NA NDOO YA MAZIWASiku moja binti wa maziwa alikuwa akitembea njiani kijijini, akiwa amebeba ndoo ya mazi...
25/07/2024

BINTI WA MAZIWA NA NDOO YA MAZIWA

Siku moja binti wa maziwa alikuwa akitembea njiani kijijini, akiwa amebeba ndoo ya maziwa kichwani. Alikuwa akitokea shambani kwake akienda kijijini kuuza maziwa aliyobeba. Wakati akiwa njiani, alianza kuota ndoto za mchana.

"Nitauza hii ndoo ya maziwa kijijini. Pesa nitakayoipata, nitaweza kununua kwa uchache angalao mayai mia tatu.
Kati ya hayo mayai mia tatu, kwa uchache mia mbili yataanguliwa na kukua hadi kuwa kuku. Nitauza sokoni kuku mia na hamsini kati ya hao mia mbili muda utakapowadia. Hamsini watakaobaki nitawatunza shambani ili watage mayai mengi zaidi.

Na nitakapoipata hii pesa nitanunua gauni zuri. Nitavaa gauni hili na kuhudhuria sherehe za Krismasi. Wanawake wote wadogo watanitamani sana na vijana wote watapenda kucheza nami muziki.
Lakini sitakuwa mwepesi. Nitatingisha kichwa na kusema hapana kwa kila mtu, hadi pale mwana mfalme mwenyewe atakaponiomba nicheze naye muziki."

Akiwa anayasema hayo, alitingisha kichwa. Mara ndoo ya maziwa ikapiga chini na yote kumwagika.

Fundisho: Usihesabu kuku wako kabla hawajaanguliwa.
Chanzo : Hadithi za Esopo

Asante kwa kusoma na kushea 🙏🙏🙏

Haijalishi wewe ni mwema au mkarimu kiasi gani; Huwezi kumridhisha mtu asiyekuwa na shukurani.
25/07/2024

Haijalishi wewe ni mwema au mkarimu kiasi gani; Huwezi kumridhisha mtu asiyekuwa na shukurani.

Utafikia yale unayoamini, yale unayoyasema, unayoyafikiri, unayojisikia(yanayokusisimua), unayoyatarajia, na unayoyafany...
22/07/2024

Utafikia yale unayoamini, yale unayoyasema, unayoyafikiri, unayojisikia(yanayokusisimua), unayoyatarajia, na unayoyafanya mara kwa mara.

22/07/2024

AINA 7 ZA WATU HATARI WA KUWAEPUKA

1. Watu Aina ya Toroli(Wheelbarow People): Aina hii ya watu hunyonya nguvu zako na hukupotezea muda. Wanatarajia uwafanyie kila kitu bila hata kujali mahitaji yako mwenyewe. Ni walaji wa nguvu zako, muda wako na rasilimali zako.

2. Watu Aina ya Mbu(Mosquito People): Watu hawa hupenda kukufaidi ilihali wao hukuingizia/hukutengenezea ubaya kwenye maisha yako. Hawana lolote jema/chanya la kukupa lakini wakati wote hutafuta kuchukua kutoka kwa wengine.

3. Watu Aina ya Kiunzi(Scaffolding People): Hawa ni watu wanaotafuta utukufu na kutawala. Wanataka kuyatawala maisha yako kwa sababu kuna wakati waliwahi kukusaidia. Wananuia kukuweka chini ya utawala wao na kuuwekea mipaka uhuru wako.

4. Watu Aina ya Mamba(Crocodile People): Hawa ni waigizaji wasiokuwa na malengo yaliyo ya kweli. Hujisogeza karibu nawe ili kujifunza siri zako na wanaweza kutumia hizo taarifa dhidi yako pale ambambo migongano itaibuka. Ni waongo, watu wanaoweza kukuumiza ikiwa hawaonekani na wasengenyaji.

5. Watu Aina ya Kinyonga (Chameleon People): Hawa ni watu wenye kijicho na wivu ambao wakati wote wapo kwenye mashindano yasiyo salama nawe. Kwa siri huwa wanafuatilia maendeleo yako wakiwa na nia hasi na hukuza sana makosa yako wakati hawakuwezeshi wala kupongeza mafanikio yako.

6. Wasema Hovyo (Naysayer People): Hawa ni wauaji wa ndoto ambao hawawezi kuthamini au kuwezesha ndoto zako. Hufokasi kwenye kufeli kwako na wakati wote huona upande hasi wa mambo, ambapo hutengeneza matatizo zaidi badala ya utatuzi.

7. Wabeba Taka (Garbage Pusher People): Aina hii ya watu huleta habari hasi na mbaya. Maisha yao yamejaa mabaki ya matatizo na husambaza habari za kukatisha tamaa na taarifa za kudhalilisha. Hupambana kusambaza taarifa mbaya na za kuvunja moyo.

Jambo la Kujifunza: Ni jukumu lako kuwatathmini watu wanaokuzunguka na kuhakikisha kuwa upo kati ya washawishi chanya. Maisha yako yataelekea kwenye mwelekeo sahihi pale ambapo utashirikiana na watu chanya na kujitenga na watu hasi.

20/07/2024

SENTENSI 8 ZITAKAZOKUZA UWEZO WAKO WA MAHUSIANO YA KIJAMII:

1. "Kutatua jambo haraka, kuwa muungwana kwa mtu anayehusika na mkali kwa tatizo lenyewe"

Unapokumbana na changamoto au migongano, chukua mtazamo unaojali hisia na maoni ya wengine na kuwa muelewa. Unapoteza nguvu kwa kumwia mkali mtu aliyekosea wakati jambo la msingi ni kutatua tatizo.

2. "Dhania kuwa kila mtu alitumwa kukufundisha kitu."

Tazama kila fursa ya kujadiliana jambo na wengine k**a fursa ya kukua na kujitambua zaidi. Mchukulie kila mtu unayekutana naye k**a mwalimu, ukitambua kuwa kila mtu ana mambo ya kukufundisha na mtizamo wa kutoa. Kuwa tayari kukubali kutokuelewana na wengine. Kuwa mdadisi.

3. "Kuwa na Vituo Unapoongea + Tazama Machoni = kujiamini."

Jenga tabia ya kuwa na vituo(pozi) kabla ya kuzungumza, hii itakupa muda wa kupanga mawazo yako na kuwa na uwasilishaji mahiri. Kutazama machoni hukuwezesha kuonesha kujiamini na kuwa mkweli.

4. "Jifunze Jinsi ya Kuwafanya Watu Wajisikie Kuwa Muhimu."

Wafanye watu wajisikie kuonekana kwa kuwapa usikivu wa kweli na uwepo wako. Hakikisha wanajisikia kuwa wamesikilizwa kwa kuwasikiliza na kuuliza maswali ya kutaka kuelewa zaidi. Kuwa na bidii ya kukumbuka taarifa za muhimu za maisha yao, mambo wanayopenda na uzoefu wao.

5. "Sauti Bora Kabisa kwa Mtu ni Ile ya Jina Lake, Hivyo Likumbuke."

Kukumbuka na kutumia jina la mtu huashiria heshima, utambuzi, na uthibitisho ambao hutengeneza hali ya kuheshimiana na kuthaminiana.
6. "Kuwa na nia njema/chanya kabla ya kutoa mrejesho."

Kabla ya kutoa mrejesho chanya wenye manufaa, ni muhimu kuhakikisha kuwa watu wengine wanajisikia kuwa unawajali na unajali mafanikio yao ya muda mrefu. Hii husaidia kuonesha nia chanya.

7. "Sifia Hadharani. Kosoa faragha."

Kutambua hadharani hujenga utamaduni wa kuthamini na kuwatambua wengine. Lakini kwa kutoa mrejesho chanya unaojenga kwa faragha, kwa heshima huunda mazingira yaliyo salama kwaajili ya majadiliano na kukua bila kuhofia kuhukumiwa na kudhalilishwa.

8. "Mategemeo ambayo hayajaelezwa ni shina/chanzo cha chuki."

Jitahidi kuelezea matarajio yako kwa namna inayoeleweka na kwa heshima la sivyo tegemea kutoelewana, chuki, na mfarakano kwenye mahusiano.

Asante kwa kusoma na kushea 🙏🙏🙏

Simtakii yeyote mabaya, lakini mtu huvuna kile anachopanda katika maisha. Huwezi kuwatendea watu k**a uchafu na ukaishi ...
19/07/2024

Simtakii yeyote mabaya, lakini mtu huvuna kile anachopanda katika maisha. Huwezi kuwatendea watu k**a uchafu na ukaishi maisha yenye furaha.

19/07/2024

SENTENSI 8 ZITAKAZOKUZA UWEZO WAKO WA MAHUSIANO YA KIJAMII :

1. "Kutatua jambo haraka, kuwa muungwana kwa mtu anayehusika na mkali kwa tatizo lenyewe"

Unapokumbana na changamoto au migongano, chukua mtazamo unaojali hisia na maoni ya wengine na kuwa muelewa. Unapoteza nguvu kwa kumwia mkali mtu aliyekosea wakati jambo la msingi ni kutatua tatizo.

2. "Dhania kuwa kila mtu alitumwa kukufundisha kitu."

Tazama kila fursa ya kujadiliana jambo na wengine k**a fursa ya kukua na kujitambua zaidi. Mchukulie kila mtu unayekutana naye k**a mwalimu, ukitambua kuwa kila mtu ana mambo ya kukufundisha na mtizamo wa kutoa. Kuwa tayari kukubali kutokuelewana na wengine. Kuwa mdadisi.

3. "Kuwa na Vituo Unapoongea + Tazama Machoni = kujiamini."

Jenga tabia ya kuwa na vituo(pozi) kabla ya kuzungumza, hii itakupa muda wa kupanga mawazo yako na kuwa na uwasilishaji mahiri. Kutazama machoni hukuwezesha kuonesha kujiamini na kuwa mkweli.

4. "Jifunze Jinsi ya Kuwafanya Watu Wajisikie Kuwa Muhimu."

Wafanye watu wajisikie kuonekana kwa kuwapa usikivu wa kweli na uwepo wako. Hakikisha wanajisikia kuwa wamesikilizwa kwa kuwasikiliza na kuuliza maswali ya kutaka kuelewa zaidi. Kuwa na bidii ya kukumbuka taarifa za muhimu za maisha yao, mambo wanayopenda na uzoefu wao.

5. "Sauti Bora Kabisa kwa Mtu ni Ile ya Jina Lake, Hivyo Likumbuke."

Kukumbuka na kutumia jina la mtu huashiria heshima, utambuzi, na uthibitisho ambao hutengeneza hali ya kuheshimiana na kuthaminiana.

6. "Kuwa na nia njema/chanya kabla ya kutoa mrejesho."

Kabla ya kutoa mrejesho chanya wenye manufaa, ni muhimu kuhakikisha kuwa watu wengine wanajisikia kuwa unawajali na unajali mafanikio yao ya muda mrefu. Hii husaidia kuonesha nia chanya.

7. "Sifia Hadharani. Kosoa faragha."

Kutambua hadharani hujenga utamaduni wa kuthamini na kuwatambua wengine. Lakini kwa kutoa mrejesho chanya unaojenga kwa faragha, kwa heshima huunda mazingira yaliyo salama kwaajili ya majadiliano na kukua bila kuhofia kuhukumiwa na kudhalilishwa.

8. "Mategemeo ambayo hayajaelezwa ni shina/chanzo cha chuki."

Jitahidi kuelezea matarajio yako kwa namna inayoeleweka na kwa heshima la sivyo tegemea kutoelewana, chuki, na mfarakano kwenye mahusiano.

Asante kwa kusoma na kushea 🙏🙏🙏

Mahusiano hufanikiwa pale ambapo watu wawili wana nia moja ya kukua pamoja.
19/07/2024

Mahusiano hufanikiwa pale ambapo watu wawili wana nia moja ya kukua pamoja.

Siyafichi makovu yangu. Ni uthibitisho kuwa nilijitokeza kuyakabili maisha. Na nilipambana.
13/07/2024

Siyafichi makovu yangu. Ni uthibitisho kuwa nilijitokeza kuyakabili maisha. Na nilipambana.

Address

NSSF Mafao House, 7th Floor , Old Moshi-Arusha Road
Arusha

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00

Telephone

+255759210560

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Epak Capital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Epak Capital:

Share