02/06/2026
with .repost
・・・
Wanawake Nane kutoka sekta mbalimbali wametunukiwa Tuzo za Malkia wa Nguvu Kanda ya Kaskazini katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa AICC Jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 ya Jukwaa la Malkia wa Nguvu.
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, Mkurugenzi wa Utalii Tanzania, Thereza Mugobi amesema jukwaa hilo limeendelea kuwa chachu ya uwezeshaji wa Wanawake kwa kuwapa fursa ya kuonesha uwezo wao na kuchangia maendeleo ya Taifa kupitia sekta mbalimbali.
Amesema Mwanamke anapopewa nafasi huleta mabadiliko makubwa si kwa maisha yake binafsi pekee, bali pia kwa familia na Jamii kwa ujumla.
Washindi wa tuzo hizo ni Leah Pantaleo Asenga (Huduma na Chakula), Dativa Koyanga (Kilimo Biashara), MWEDO – Maasai Women Development Organization (Afya na Ustawi wa Jamii), Mariam Chuma Kobelo (Utumishi Bora Sekta ya Umma), Miriam Oscar Kaaya (Elimu, Malezi na Ulinzi wa Mtoto), Christine Mwakatobe (Diplomasia ya Uchumi na Utalii), Carolyn Kandusi (Mapinduzi ya Kidigitali na Maendeleo ya Jamii) pamoja na Mary Msonsa (Biashara, Uvumbuzi na Ajira).
Humbled 🙏🏽