31/01/2025
Gavana Benki Kuu akoshwa ushirikiano wa ZEEA na Airpay kuwafikia wakopaji
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Emmanuel Tutuba amependa ushirikiano unaofanywa baina ya Kampuni Airpay Tanzania na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) katika kuwafanya wananchi kurejesha mikopo ya bila riba inayotolewa na Serikali ya Zanzibar.
Ushirika huo wa ZEEA na Airpay ambayo ni Kampuni yenye lengo la kurahisisha mifumo ya malipo ya kifedha kidijitali kwa watu wa kawaida Wafanyabiasha na wajasiliamali wadogo wadogo inaelezwa kuwa utasaidia wakopaji kurejesha na kukopa fedha kwa wakati.
Gavana Tutuba ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha BoT, ZEEA, Airpay pamoja na wadau mbalimbali kutoka Taasisi za kibenki ambazo ni Benki ya Taifa ya Biashara (TCB), Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) na mitandao ya simu ambayo ni Airtel, Mix by Yas, MPesa, Duns and Bradstreet na Creditlnfo.
Alisema amefurahi kuona ZEEA wanashirikiana na Airpay katika kuleta mfumo wa kidijitali ili kusaidia namna nzuri ya kuwafanya wakopaji kurejesha fedha zinazotolewa na serikali bila riba ili ziweze kusaidia wananchi wengine na kwamba imani yake mfumo huo utasaidia urejeshwaji wa pesa hizo.
Naye Mihayo Wilmore kiongozi upande wa Mifumo kutoka Airpay Tanzania alisema kitu wanachotaka kukifanya ni kuweza kuhakikisha mteja hapati usumbufu katika urejeshaji.
"Mtumiaji anaweza kwenda kwa wakala yoyote kulipa bila usumbufu wowote changamoto ni mkopo unaochukuliwa na kushindwa kurejeshwa unakuwa mkopo chechefu sasa tumekuja kuomba Benki Kuu ya Tanzania ituruhusu kuchukua asilimia 33 ya kile ambacho kipo kwenye simu ya mteja ili aweze kurejesha kidogo kidogo k**a ulikuwa na sh 10,000 tutachukua sh 3,000 kukupunguzia deni lako la sh 100,000,"alisema.
Juma Burhan Mohamed Mkurugenzi Mtendaji ZEEA alisema, wao k**a wakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi washatoa mikopo yenye thamani ya sh Bilioni 34.9 ambao umewafikia wanawake 14,000 na wanaume 9,000.
"Utoaji unakwenda vizuri kuanzia 2022 hadi 2024 lakini hili la mtandaoni ni jambo zuri maana mambo yako huko kwa sasa tumeona kuna haja ya kukaa pamoja na kuweza kuona sisi k**a wakala kwa kushirikiana na t