25/04/2026
Tujifunze kujitazama k**a miti, na kuwatazama wengine kwa mtazamo huo pia...usikasirikee😁, kaa chini nikueleweshe 🧘
Kila mti una thamani yake...🤔
Kuna mti utakupa kivuli tu bila matunda,
mwingine utakupa matunda bila kivuli,
mwingine maua mazuri bila kivuli wala matunda,
na kuna ule adimu unaokupa vyote kwa pamoja.
Vivyo hivyo na watu, kila mmoja ana mchango wake, kwa namna yake..
Usimlaumu mti kwa kutokupa matunda ikiwa asili yake ni kivuli tu.
Usitarajie maua kwa ule ulioumbwa kutoa matunda pekee.
Kila mmoja ameumbwa na nafasi yake: punguza lawama, ongeza uelewa..✍️✍️
Pia tambua kuwa, kuna misimu maishani.📈📈
Kuna kipindi cha kiangazi ambapo miti hunyauka na kupukutisha majani yake; hiki ni k**a nyakati ngumu, kushuka kiuchumi au kupitia changamoto za maisha.
Na kuna kipindi cha masika ambapo miti huchanua, hustawi na kuwa yenye uzuri wa kuvutia; hiki ni k**a nyakati nzuri ambapo mambo huenda sawa na kila kitu huonekana kujaa baraka.
Kumbuka pia, si kila mti ni salama😁😁, Kuna miti yenye sumu, na mingine ni dawa, Kuna inayovutia wadudu au hata wanyama wakali; hivyo chagua kwa umakini unachokikaribia.✍️✍️
Na mwisho, miti ikiwa mingi sana bila mpangilio, huweza kuunda kichaka kinachoficha hatari.
Ndivyo ilivyo pia kwa ushauri mwingi usiochujwa, unaweza kukupoteza badala ya kukuongoza.✍️
Chagua kwa hekima, elewa kwa kina, na ishi kwa utulivu.🪢