03/03/2021
FAIDA ZA MAFUTA N**I PIKI MWILINI.
1. Mafuta ya n**i kwa afya ya Moyo:
Mafuta ya n**i yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu k**a High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu k**a Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo k**a anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum.
2. Mafuta ya n**i huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula:
Hii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya n**i niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya n**i yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi k**a yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo wa mwili kukimeng’enya chakula, watu wanaoyatumia mafuta haya kupikia vyakula vyao kila siku kwa kawaida huwa na uzito wa kawaida. Anasema Geeta Sidhu Robb, mtaalamu wa lishe na mwanzilishi wa Nosh Detox.
3. Mafuta ya n**i hung’arisha ngozi:
Siyo sehemu za ndani tu ya mwili zinazofaidika na mafuta haya ya n**i k**a yanavyofanya mafuta mengine ya asili, k**a unataka kuwa na ngozi nzuri yenye mng’aro na yenye afya na yenye muonekano wa asili basi paka mafuta ya n**i kila siku kwenye ngozi yako, mafuta ya n**i yana uwezo mkubwa katika kuua bakteria, virusi, na vijidudu vya aina yeyote vinavyoweza kuidhuru ngozi, haya ni mafuta kwa mwili mzima yaani pakaa kwenye ngozi yote usoni, mwilini, kwenye nywele na kwenye kucha. Pia unaruhusiwa kuyatumia mafuta haya wakati wa masaji.
4. Huongeza nguvu mwilini:
Mafuta ya n**i ni chanzo kizuri cha nguvu ya mwili kwani yana sifa ya kuelea kwa kiasi kidogo kwenye damu ‘medium chain triglycerides .
Wasiliana Nasi WhatsApp: 0659432215 au 0764013664.
NB: 100% pure N**i.